Maalim Seif: Lipumba mnafiki, mpotoshaji .....soma habari kamili na matukio360....#share
Na Abraham Ntambara,
Dar es Salaam
KATIBU Mkuu wa Chama
cha Wananchi CUF Maalim Seif amedai Profesa Ibrahim Lipumba ni mpotoshaji, mnafiki na amekisaliti chama.
Pia Maalim Seif amekanusha kuwa yeye ndiye anayekidhoofisha chama na kwamba lengo la Profesa Lipumba si kujenga chama bali kukichafua.
Pia Maalim Seif amekanusha kuwa yeye ndiye anayekidhoofisha chama na kwamba lengo la Profesa Lipumba si kujenga chama bali kukichafua.
Katibu Mkuu wa CUF Maalim Sief akizungumza katika kongamano la chama lililofanyika wilayani Kinondoni kata ya Tandale jijini Dar es Salaam.
Juzi Profesa Lipumba
akizungumza na waandishi wa habari alidai katibu mkuu huyo amekidhoofisha CUF kwa kutotekeleza azimio la
baraza kuu la kufungua kesi mahakama kuu ya Zanzibar kupinga kufutwa matokeo ya
uchaguzi wa wakilishi na madiwani wa Oktoba 25, 2015.
Pia alidai mgogoro unaoendelea ndani ya chama cha CUF
ulianzishwa na Maalim Seif Sharif akiwa na lengo la kudhoofisha chama hicho na
kuwakumbatia viongozi wa Chadema.
Maalim Seifa akizungumza
jana katika kongamano la chama lililokuwa na lengo la kubadilishana mawazo juu
ya hali, mwenendo na matatizo ya chama ili kuyatafutia ufumbuzi lililofanyika
wilayani Kinondoni kata ya Tandale jijini Dar es Salaa, alisema madai hayo ni
upotoshwaji.
“Anasema eti
mgogoro uliopo ni mimi kung’ang’ania viongozi wa Chadema ni mnafiki mkubwa,
aliyeunda Ukawa ni yeye mwenyewe, mtoto aliyemzaa mwenyewe anataka kumuua,
Lipumba amekisaliti chama na asimtafute mtu wakumbebesha maiti,” amesema
Maalim. Na kuongeza "lengo la Profesa Lipumba si kujenga chama bali kukichafua."
Akijibu kuhusu
madai kutotekeleza maazimio ya baraza kuu ya kufungua kesi mahakama kuu
Zanzibar kupinga kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi ili kuundwa kwa serikali ya
umoja wa kitaifa, amesema kuwa hakuna maazimio kama hayo.
Katibu
mkuu huyo amesema lengo la CUF ni kuongoza serikali ni si kuunda serikali ya
umoja wa kitaifa kwani hata akiwa katika serikali hiyo bado itaongozwa na ilani
ya chama chenye rais.
Katika
hatua nyingine Maalim ameendelea kusisitiza kuwa CUF ilishinda uchaguzi wa urais
wa Oktoba 25, 2015 na kudai kuwa uchaguzi wa marudio ni haramu na serikali
iliyopo ni haramu hivyo haitambui na hawezi kushirikiana nayo.
Amesema kwamba
wataendelea kudai haki ya wazanzibar, na anaamini itapatikana kwa uwezo wa Mwenyezi
Mungu.
No comments:
Post a Comment