Manispaa ya Ilala kutumia bilioni 287 .....soma habari kamili na matukio369....#share


Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

HALMASHAURI ya Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam, imepitisha bajeti ya sh.bilioni 287 kwa mwaka wa fedha 2018/2019 kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo na matumizi ya kawaida.
Baraza la Madiwani Halmashauri ya Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam likipitisha bajeti ya mwaka wa fedha 2018/2019.

Akizungumza na waandishi wa habari kwa niamba ya Mkurugenzi baada ya kupitishwa kwa bajeti hiyo, Mchumi wa Ilala Ando Mwanduga, amesema fedha hizo zimegawanyika katika makundi mawili.

“Lakini katika bilioni 287 imegawanyika, kuna fedha za ruzuku pamoja na mapato ya ndani,” amesema Mwanduga.

Ameeleza bajeti ya mapato ya ndani yanayotokana na vyanzo vya halmashauri ni sh.bilioni 56.8 na kwamba fedha inayobaki inatokana na ruzuku kutoka serikalini.

Amesema kama ilivyo maelekezo ya serikali kwa mapato ya ndani wametenga asilimia 60 kwa ajili ya miradi ya maendeleo na asilimia 40 kwa ajili ya matumizi ya kawaida.

“Sasa ukikokotoa hapo unapata kwamba kwenye miradi ya maendeleo ipo sh.bilioni 35 na bilioni kama 24 zipo kwa matumizi ya kawaida,” amesema.

Mwanduga amesema bajeti hiyo imeongezeka kutoka sh.biloni 124 kwa bajeti iliyopita hadi sh.287 ya mwaka huu wa fedha 2018/2019.

Awali akiwasilisha mapendekezo ya mipango na bajeti Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi na Huduma za Jamii Jacob Kissi amesema kamati yake inataraijia kutumia jumla y ash.bilioni 122.9.

“Sh.bilioni 95.3 kwa ajili ya mishahara, sh.bilioni 8.1 kwa matumizi ya kawaida na bilioni 19.4 kwa ajiliya miradi ya maendeleo,” amesema Kissi.

Ametaja miradi ya maendeleo itakayotekelezwa kuwa ni katika elimu ya msingi,Idara ya elimu ya sekondari, Idara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika, Idara ya Afya na Ustawi wa Jamii.

Mingine ni Idara ya Maendeleo ya Jamii ya Vijana na Idara ya Mifugo na Uvuvi.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search