Mbunge Mary Nagu ashikiliwa na polisi.... soma habari kamili na matukio360...#share
Na mwandishi wetu, Hanang
Mbunge wa Hanang (CCM), Dk Mary Nagu anashikiliwa na jeshi la polisi akidaiwa kuichonganisha serikali na wananchi.
Dk Mary Nagu
Dk Nagu aliyewahi kuwa waziri katika wizara kadhaa wakati wa utawala wa Serikali za awamu mbili zilizopita, anashikiliwa na polisi kwa agizo la mkuu wa wilaya ya Hanang, Sara Msafiri.
Mkuu huyo wa wilaya ameiambia matukio360 kuwa hatua hiyo inafuatia mbunge huyo kuhamasisha wananchi wasichangie wala kujishughulisha na shughuli za maendeleo.
" Nimeagiza akamatwe kwa kuwa anawashawishi wananchi wasichangie wala kujishughulisha na shughuli za maendeleo, hivyo unapozuia jitihada za maendeleo maana yake unaichonganisha serikali na wananchi," amesema
Pia amesema mbunge huyo amekuwa akihamasisha wananchi wasishiriki shughuli zinazofanywa na mkuu huyo wa wilaya.
Hata hivyo mkuu wa wilaya hiyo ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya siasa ya wilaya(CCM) amesema Nagu ataachiliwa mara baada ya taratibu kukamilika.
Mbunge wa Hanang (CCM), Dk Mary Nagu anashikiliwa na jeshi la polisi akidaiwa kuichonganisha serikali na wananchi.
Dk Mary Nagu
Dk Nagu aliyewahi kuwa waziri katika wizara kadhaa wakati wa utawala wa Serikali za awamu mbili zilizopita, anashikiliwa na polisi kwa agizo la mkuu wa wilaya ya Hanang, Sara Msafiri.
Mkuu huyo wa wilaya ameiambia matukio360 kuwa hatua hiyo inafuatia mbunge huyo kuhamasisha wananchi wasichangie wala kujishughulisha na shughuli za maendeleo.
" Nimeagiza akamatwe kwa kuwa anawashawishi wananchi wasichangie wala kujishughulisha na shughuli za maendeleo, hivyo unapozuia jitihada za maendeleo maana yake unaichonganisha serikali na wananchi," amesema
Pia amesema mbunge huyo amekuwa akihamasisha wananchi wasishiriki shughuli zinazofanywa na mkuu huyo wa wilaya.
Hata hivyo mkuu wa wilaya hiyo ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya siasa ya wilaya(CCM) amesema Nagu ataachiliwa mara baada ya taratibu kukamilika.
No comments:
Post a Comment