Meya Mwita ataka halmashauri kutoa ajira kwa watakaozika maiti... soma habari kamili na matukio360....#share
Na Mwandishi Wetu, Dar
es Salaam
MEYA
wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita amezitaka halmashauri zote za jiji hilo kuajiri watumishi ambao watakuwa wanafanya kazi ya kuzika
miili ya watu ambao hawana ndugu.
Meya Mwita ametoa kauli hiyo leo kwenye kikao cha robo ya pili ya Baraza la Madiwani wa Jiji la
Dar es Salaam ,ambapo amewaeleza madiwani hao kuwa jukumu la kuzika
marehemu wasiokuwa ndugu ni la jiji,kwakushirikiana na halmashauri hivyo wanapaswa
kuwajibika katika hilo.
Amefafanua hadi sasa jiji limeshanunua gari pamoja na mahitaji mengine ya kuhifadhia
miili hiyo pindi inatokea na kwamba changamoto iliyopo ni watu ambao
watashirikiana kutekeleza jukumu hilo.
“ Mtakuabliana na mimi kwamba tulishakubaliana
kwamba jambo hili lifanyike kwenye halmashauri zetu, lakini hadi sasa
Kinondoni pekee ndio wametimiza agizo hili, sasa ninaagiza tena halmashauri
nyingine za jiji hili kuajiri watu hao” amesema Mwita.
Mwita amesema kuwa Halmashauri ya
Jiji la Dar es Salaam pamoja na halmashauri nyingine zilizopo jijini hapo
walikubaliana kuzika watu wasiokuwa na ndugu hivyo kila mmoja anapaswa
kutekeleza makubaliano hayo.
“Hivyo marehemu wanapokuwa
wamekaa muda mrefu wanalazimika kuzikwa na jiji, natulikubali kuchangia
usafiri,dawa na sanda,” amesema.
Amefafanua kuwa watu
wasiokuwa na ndugu wanapokufa, wanapokaa hospitalini zaidi ya siku
20,jiji linalazimika kuwazika hivyo wapo ambao wanazikwa kwenye halmashauri
mbalimbali.
Hivyo wakati Jiji la Dar es
Salaam likitimiza wajibu wake katika kuzika marehu hao kila halmashauri
linajukumu la kutoa watumishi kwa ajili ya kuzika.
Amefafanua taarifa alizonazo ni
Halmashauri ya Kinondoni pekee ndio ambayo imeajiri watumishi kwa ajili ya
kuzika miili ya watu ambao wamefariki na hawana ndugu.
“Ni wajibu wa halmashauri
kuhakikisha wanafanikisha kupatikana kwa watumishi hao haraka,” amesema Mwita.
No comments:
Post a Comment