Nape: Mwenyezi Mungu aliniokoa na mdomo wa bunduki...soma habari kamili na matukio360...#share

 Na Mwandishi

MBUNGE wa Mtama kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye amesema Mwenyezi Mungu alimuokoa na mdomo wa bunduki wa wanyama wasiopenda haki.

Amesema hay oleo kupitia ukurasa wake wa twitter ikiwa leo ni mwaka mmoja tangu alipotolewa bastola wakati akitaka kuzungumza na waandishi wa habari nje ya Hoteli ya Protea muda mfupi baada ya kutenguliwa nafasi yake kama Waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo.

Nape ameandika, “mwaka mmoja uliopita tarehe kama ya leo Mwenyezi Mungu aliniokoa na mdomo wa bunduki wa wanyama wasiopenda haki! Mungu mkubwa, mbegu ya haki haifi.”

Katika ujumbe huo Nape ameweka picha yake ya video akizungumza na waandishi wa habari nje ya hoteli hiyo kueleza masuala mbalimbali, huku akiwataka vijana kudai haki zao bila woga.

Mtu aliyemtishia bastola Nape alikuwa pamoja na wenzake wawili ambao kwa pamoja walikuwa wakimlazimisha arudi kwenye gari lake na kuondoka, lakini mbunge huyo aligoma na ndipo (mtu huyo) aliporudi nyuma na kuchomoa bastola kutoka kiunoni  kisha kumtishia kabla ya kutulizwa na mwezake.

Baada ya tukio hilo watu hao walitoweka eneo hilo muda mfupi baadaye.

Kufuatia tukio hilo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba alisema mtu aliyemtishia bastola Waziri huyo wa zamani wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo hakuwa askari wa Jeshi la Polisi.


Mwaka mmoja uliopita tarehe kama ya leo Mwemyezi Mungu aliniokoa na mdomo wa bunduki wa wanyama wasiopenda haki! Mungu mkubwa, mbegu ya haki haifi!

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search