Watano wafariki, wengine wajeruhiwa katika ajali Morogoro...soma habari kamili na matukio360...#share



Na mwandishi wetu, Morogoro

WATU watano, wanawake wanne na mwanaume mmoja wamepoteza maisha katika ajali iliyohusisha basi la New force T 346 DLY iliyokuwa ikitokea Dar kuelekea Tunduma na Hiace T 962 BSE iliyokuwa ikitokea kijiji cha Mlali kuelekea mjini Morogoro.


Ajali hiyo imetokea jana saa 4.15 asubuhi eneo la Lungenba, kilometa chache kutoka Msamvu kuelekea Iringa.

RTO wa mkoa wa Morogoro Boniphace Mbao amesema majeruhi wa ajali hiyo ni 12 ambao wamelazwa katika hospitali ya mkoa wa Morogoro.

Chanzo cha ajali ni dereva wa Hiace kujaribu kuyapita magari mengine bila tahadhali na kwenda kugongana uso kwa uso na basi hilo. Dereva wa Hiace amepoteza maisha.


Picha mbalimbali za ajali iliyotokea leo Mkoani Morogoro ikihusisha gari la Kampuni ya New Force na gari dogo aina ya Hiace









About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search