Samia aagana na mabalozi wa Tanzania nchini Rwanda, Urusi...soma habari kamili na matukio360...#share


Na Mwandishi Wetu, Dodoma

MABALOZI wa Tanzania Nchini Rwanda Ernest Mangu na Meja Jenerali Mstaafu Simon Marco Mumwi  wa  Urusi leo wamekutana na kuzungumza na Makamu wa Rais wa  Samia Suluhu Hassan mjini Dodoma.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini Urusi Mhe. Jenerali Mstaafu Simon Marco Mumwi pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Rwanda Mhe. Ernest Mangu ambao walifika nyumbani kwa Makamu wa Rais kwa lengo la kumuaga kwenye makazi yake Kilimani mjini Dodoma.

Mabalozi hao walifika kwenye makazi ya Makamu wa Rais, Kilimani Dodoma  kwa lengo la kumuaga ,walimuahidi Makamu wa Rais kufanya kazi kwa ajili ya Tanzania.

Wamemuambia Makamu wa Rais wanajua dhamana kubwa waliopewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na dhamira yake ya Tanzania ya Viwanda .

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja  na Balozi wa Tanzania nchini Urusi Mhe. Jenerali Mstaafu Simon Marco Mumwi pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Rwanda Mhe. Ernest Mangu ambao walifika nyumbani kwa Makamu wa Rais kwa lengo la kumuaga kwenye makazi yake Kilimani mjini Dodoma.

Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search