SERIKALI:Unyanyasaji kijinsia unaathiri tabaka zote...soma habari kamili na matukio360...#share


Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

SERIKALI amesema ukatili dhidi ya wanawake unaathiri matabaka yote na viwango vya ukatili vya kimwili, kingono na kisaikolojia vipo juu zaidi vijijini na miongoni mwa wale wenye elimu ya chini
Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP-Mtandao Lilian Liundi akizungumza na waandishi wa habari wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyoandaliwa na mtandao huo.

Hayo yamesemwa jana jijini Dar es Salaam na  katibu wa wizara ya afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto Sihaba Nkinga katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyoandaliwa na TGNP-Mtandao.

“Takwimu zinaonesha karibu wanawake wanne kati ya kila 10 wamewahi kunyanyaswa huku asilimia 20 wakifanyiwa ukatili wa kijinsia kwenye maisha yao,” amesema Nkinga.

Amesema katika mapitio ya ukatili dhidi ya watoto ya mwaka 2011, imeonekana mmoja katika ya kila wasichana watatu, na mmoja katika kila wavulana saba wanapitia aina moja au nyingine ya ukatili wa kijinsia kabla ya kufikia umri wa miaka 18.

Nkinga amesema ukatili dhidi ya wanawake unaathiri matabaka yote, na viwango vya ukatili vya kimwili, kingono na kisaikolojia vilikuwa juu zaidi vijijini na miongoni mwa wale wenye elimu ya chini.

Amesema katika kukabiliana na vitendo hivyo serikali kwa kushirikiana na wadau imeandaa mpango wa taifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto 2017/2018-2021/22 mpango ambao umekwishaanza utekelezaji wake.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP-Mtandao Lilian Liundi, amesema mada kuu katika maadhimisho hayo kidunia ni “Sukuma Mabadiliko kuelekea usawa wa jinsi,” ambapo msisitizo ni kutomuacha mtu nyuma yaani twende wote huku kitaifa yakiongozwa na mada kuu isemayo “Kuelekea uchumi wa viwanda: Tuimarishe usawa wa jinsia na uwezeshaji wanawake vijijini.”

Amesema wanawake ni mgongo wa maendeleo vijijini na uchumi wa nchi. amesema “Takwimu za UN Women zinaonesha kuwa wanawake ni asilimia 43 ya nguvu kazi ya kilimo duniani, ambayo kwa nchi nyingine inapanda hadi asilimia 70. Kwa upande wa Afrika kilimo kinafanywa kwa asilimia 80 na wakulima wadogo wadogo ambao wengi wao ni wanawake.

Amesema pamoja na mchango mkubwa wa wanawake katika sekta ya kilimo, bado wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo umasikini na kutokumiliki adhi na asilimali za uzalishaji. Takwimu zinaonesha takribani asilimia 60 ya wanawake ni masikini hususani wale wa vijijini.

Liundi amesema katika kusisitiza ushiriki wa wanawake katika Tanzania ya viwanda inatakiwa kuzingatiwa kanuni (principal) ya malengo endelevu ya dunia ya kutomwacha mtu nyuma kwa kufanya uchambuzi wa kina kwa jicho la jinsia ili kuleta ushiriki jumuishi na wenye tija.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search