Tahliso waibua tena sakata kifo cha Akwilina...soma habari kamali na matukio360...#share


JUMUIYA YA TAASISI ZA VYUO VYA ELIMU YA JUU TANZANIA (TAHLISO) OFISI YA MWENYEKITI TAHLISO

TAARIFA KWA UMMA.

Mwenyekiti wa Tahlisi George Albert  Mnali  wa pili kutoka kulia akizungumza na baraza Kuu la Senate leo  kushoto ni Katibu Mkuu wa Tahliso John Mboya kulia ni Katibu wa Baraza hilo Faidhaa Msangi na kulia ni Kaimu Makamu Mwenyekiti wa Rais wa Chuo cha Zanzibar University

Ndugu    waandishi wa habari tunawashukuru sana kwa kukubali wito wetu wakuja kujumuika pamoja na sisi.

Leo tarehe 3/3/2018 tumekuta na viongozi wa vyuo vikuu nchi nzima kwa ajili yakujadili changamoto zinazotukabili. Kikao hiki ni cha TAHLISO BarazaKuu (SENATE) kinacho husisha Maraisi wa serikali za wanafunzi wa VyuoVikuunchini.

Tunatambuakwambakunakifo cha mwanafunzi mwenzetu Akwilina Akwilini,mwanafunziwachuo cha NIT kilichotokea mwezi wa pili.

Tunawashukuruwanafunziwenzetukwautulivumkubwanamshikamanowaliouoneshatangumsibaulipotokea, wakatiwakipindi cha majonzihadikufikiasasa.

TunamshukuruMhe.Raisi wa Jamuhuri ya Muunganowa Tanzania kwa kuingilia kati suala hili na kuagiza uchunguzi ufanyike na hatua za kisheria zichukuliwe kwa wote watakaobainika kuhusika na kifo cha AkwilinaAkwilini. 
Vilevile tunaishukuru WizarayaElimu, Sayansi na Teknolojia kwa ukaribu waliouonesha katika kipindi chote cha msiba.Tunaomba wanafunzi waendelee kuwa watulivu wakati maagizo ya Rais yakitekelezwa.

Aidha tunapenda jamiii tambue kuwa TAHLISO ndio chombo kikuu cha kuwasemea wanafunzi wote nchi nzima Tanzania na sio kikundi kingine chochote kile. 

Vipo vikundi vingivi mejitokeza na kutoa matamko mbalimbali baada ya kifo hiki kutokea, vikundi vingine vikaenda mbali Zaidi kwa kuwataka baadhi ya watendaji wa Serikali akiwemo Waziri wa Mambo ya Ndani kujiuzulu jambo ambalo linaashiria vikundi hivyo kuongozwa ama kutumika namakundi ya kisiasa, haiwezekani kutaka watendaji wa Serikali wajiuzulu wakati uchunguzi bado unafanyika na matokeoya uchunguzi huo bado hayajatoka.

Tunatoa wito kwa vikundi vyote vinavyojihusisha na kutumia mwamvuli wa Marais waVyuoVikuu kama kinga yao ili kuu hadaa Umma kwamba wanaungwa Mkono, vikundi hivyo viache tabia hiyo vinginevyo tutawachu kulia hatua za kinidhamu.

TAHLISO tunasubiri matokeo ya Uchunguzi unaofanyika juu ya kifo cha Akwilina na tunaimani wahusika wote watachukuliwa hatua kali zakisheria. 
Tunawaombawanafunzi wote tuendelee kuwa watulivu wakati tukisubiri matokeo hayo na kujiepusha na maandamano na vitendo vyovyot e vitakavyo sababisha uvunjifu wa Amani nakuleta mgawanyo miongoni mwawanafunzi.        
                                                                                          Hata hivyo namna bora yakufikisha hoja nikutumia njia ya majadiliano kama wasomi badala ya kutumia nguvu ama maandamano kwakutofuata taratibu na madhara yake ni kusababisha vuruguzi sizotakiwa na hatimaye kuhatarisha usalama na hivyo kuathiri jamii kwaujumla wake.

Vurugu zozote zitokanazo kwa kutozingatia taratibu zinaweza kudhorotesha shughuli za kiuchumi kwa mtu mmoja mmoja na Uchumiwa Taifa letu. Vile vile zinapoteza mvuto kwawawekezaji wanje na wandani, ikiwemo shughuli za utalii nchini ambazo zinachangia pato la Taifa letu.                                                                
  
Athariza Vurugu na kukosekana kwa amani zipo wazi natunaziona kwa nchi nyingine zikiwemo baadhi ya nchi jirani zetu ambao wamekua wakimbizi nchini kwetu kila siku.

Tunaona kuwa kama wanataaluma tunajukumu kubwa la kuelimisha jamii na kuwamfano bora wakutumia njia za majadiliano katika kujenga hoja zetu ilizitatuliwe kuliko kutumia njia ya maandamano au vurugu zisizo na ulazimawowote.
Taasisi hii ndio yenye dhamana ya kutetea nakusimamia maslahi ya wanafunzi wote wa vyuo na vyuovikuu Tanzania na si vinginevyo.
………………………………….
GEORGE ALBERT MNALI
MWENYEKITI TAHLISO


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search