Ujenzi nyumba za polisi Arusha wakamilika....soma habari kamili na matukio360...#share

Na Mwandishi Wetu, Arusha
UJENZI wa nyumba mpya za makazi ya askari polisi mkoani Arusha umekamilika. Hutua hiyo ilifuatia baada ya mwaka jana moto kuteketeza nyumba zilizokuwepo eneo hilo.
Makazi mpya ya nyumba za askari polisi mkoani Arusha
Hatua hiyo imeridhiwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi Dk. Mwigulu Nchemba alipokagua ujenzi wa nyumba hizo za kisasa.
Dk Mwigulu amempongeza rais John Magufuli, mkuu wa Mkoa huo, Mrisho Gambo na wafanyabiashara mkoani humo kusaidia ujenzi wa nyumba hizo.
"Leo hii mmeona nyumba hizi za kisasa ambazo zitafanya askari wangu kuanza kupigia selfie katika nyumba zao kwamba hapa ndipo ninapokaa, ili ni jambo kama waziri na mshukuru sana Rais na litaongeza morali ya kuendelea kufanya kazi nzuri wanavyofanya, " amesema Mwigulu.
Mrisho Gambo akimueleza jambo Waziri Mwigulu alipokagua ujenzi wa nyumba za askari polisi
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa huo, Gambo amemshukuru waziri Mwigulu kwa msaada wake wa kufanikisha ujenzi huo ikiwamo kukagua kila hatua ya ujenzi.
Pamoja na mambo mengine Mwigulu amekubali kupeleka gari la polisi katika kituo cha Murieti ili kupunguza matukio ya kihalifu kufuatia ongezeko la watu katika eneo hilo.
UJENZI wa nyumba mpya za makazi ya askari polisi mkoani Arusha umekamilika. Hutua hiyo ilifuatia baada ya mwaka jana moto kuteketeza nyumba zilizokuwepo eneo hilo.
Makazi mpya ya nyumba za askari polisi mkoani Arusha
Hatua hiyo imeridhiwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi Dk. Mwigulu Nchemba alipokagua ujenzi wa nyumba hizo za kisasa.
Dk Mwigulu amempongeza rais John Magufuli, mkuu wa Mkoa huo, Mrisho Gambo na wafanyabiashara mkoani humo kusaidia ujenzi wa nyumba hizo.
"Leo hii mmeona nyumba hizi za kisasa ambazo zitafanya askari wangu kuanza kupigia selfie katika nyumba zao kwamba hapa ndipo ninapokaa, ili ni jambo kama waziri na mshukuru sana Rais na litaongeza morali ya kuendelea kufanya kazi nzuri wanavyofanya, " amesema Mwigulu.
Mrisho Gambo akimueleza jambo Waziri Mwigulu alipokagua ujenzi wa nyumba za askari polisi
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa huo, Gambo amemshukuru waziri Mwigulu kwa msaada wake wa kufanikisha ujenzi huo ikiwamo kukagua kila hatua ya ujenzi.
Pamoja na mambo mengine Mwigulu amekubali kupeleka gari la polisi katika kituo cha Murieti ili kupunguza matukio ya kihalifu kufuatia ongezeko la watu katika eneo hilo.
No comments:
Post a Comment