Mauaji nchini serikali yatakiwa kutoa tamko...soma habari kamili na matukio360...#share
Na Abraham Ntambara,
Dar es Salaam
SERIKALI imetakiwa kutoa
tamko dhidi ya vitendo vya kupotea na kuuawa kwa watu nchini.
Mshauri wa masuala ya jinsia, mwanaharakati wa haki za binadamu na huduma ya jamii (Tamwa) Gemma Akilimali akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Pia imetakiwa kuwa na
uvumilivu kwa kuacha kuwanyamazisha watu wanaotumia uhuru wao wa kikatiba kutoa
matamko na maamuzi juu ya serikali ilimradi wasivunje sheria za nchi.
Kauli hiyo imetolewa
jana jijini Dar es Salaam na Mshauri wa masuala ya jinsia, mwanaharakati wa haki za binadamu na huduma ya jamii (Tamwa) Gemma Akilimali alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, amesema vitendo hivyo ni ishara ya amani na
usalama kuanza kuyeyuka nchini.
Amesema “Serikali
haioneshi kuhusika na matukio haya, lakini ni kwa nini iko kimya?, Tunaamini
kwamba inajua na inaendelea kujua tunaomba serikali iwajibike kutoa matamko na
kufuatilia usalama wa raia ili kuwe na hiyo amani ambayo inataka kuanza
kuyeyuka,” amesema Akilimali.
Amesesitiza kwa kusema
kuwa serikali inatakiwa kuwajibika katika kusimamia amani, usalama na haki ya
kuishi kwa binadamu ambapo ameongeza kwamba kama amani itakosekana tutakuwa
tumepoteza tunu muhimu sana.
Mwanaharakati huyo
amesema kwa sasa kunaviashiria vya
matukio ya kuanza kupotea amani ndiyo sababu sauti zinaanza kujitokeza kuidai ambapo
ameeleza kwamba kwa sasa kuna mmomonyoko mkubwa wa amani na hasa kutokana
serikali kushindwa kusikiliza sauti za watu.
“Kwa sasa kuna tatizo
linalojitokeza na kummomonyoka kwa amani na sababu ni serikali kushindwa kusikiliza sauti na sisi huwa tunaamini sauti inaleta
ajenda, unaponyamanzisha sauti unakosa ajenda,” amesema.
“Lakini vilevile
matukio mbalimbali ambayo yanatokea na hasa yale yanayosababisha sasa mpaka
watu kupotea ukisema hiki tayari unapotea pamoja na vifo visivyotaraiwa
vinavyotokea ni hofu inayoanza kutawala nchini,” amesema.
Ametoa msisitizo kwa
serikali kuvumilia wanaoikosoa kwa kusema “Kwa hiyo serikali tunaiomba
ivumilie, wale ambao wanataka kusema chochote ila wasivunje sharia, kwa hiyo
sisi tunaomba uvumilivu wa serikali,”
Amesema njia
zianzotumia kwa sasa siyo zile abazo zilikuwa zinaendeleza amani bali ni zile
ambazo zinaichokonoa amani na kwamba kama kunawatu wanakosea wanatakiwa wapelekwe
mahakamani ili mahakama iweze kuamua.
No comments:
Post a Comment