Uvccm wamchokonoa Waziri Mwakyembe.... soma habari kamili na matukio360...#share


Na Mwandishi Wetu, Dodoma

MWENYEKITI wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Kheri Jemes amewataka viongozi wenye mamlaka ya kusimamia tasnia ya sanaa na utamaduni nchini kuacha kufanya kazi ya uhakimu.

 Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Kheri James

Kauli hiyo imekuja mwezi mmoja baada ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kusitisha kuchezwa kwa nyimbo 15 za wasanii mbalimbali kwa kile kilichodaiwa ni nyimbo hizo kutokuwa na maadili ya kitanzania.

Akizungumza jana mjini Dodoma na wanachama wa umoja huo, James amewataka viongozi wenye mamlaka hayo kuwaelimisha wasanii nini cha kufanya ili kuboresha badala ya kufungia tu.

“Viongozi wanaoshughulika na masuala ya sanaa na utamaduni wasiifanye kazi hii kama kazi ya uhakimu bali waifanye kama kazi ya ualimu kwa kuwafundisha watu namna ya kufanya”- amesema James.

“Serikali ya CCM imeahidi ajira kwa vijana, Vijana wameamua kujiajiri kwenye sanaa. Walimu wetu ni kuwawezesha kwenye sanaa na sio kuwakatisha tamaa kwahiyo tusitumie kigezo cha sheria na taratibu kuwaangamiza watu ambao tungeweza kuwaelimisha na wakafanya vizuri zaidi,” ameongeza.

“Leo tuna wasanii ambao wameitangaza nchi yetu vizuri na wanalipa kodi kwa kazi zao sasa leo tunataka kupoteza mabalozi wazuri na walipakodi kwa makosa madogo ambayo yanaweza kurekebishwa na tukaendelea kufanya vizuri. Kama tutaaendelea kuwaacha vijana wakiangamizwa kwa kitu kinaitwa kanuni na taratibu za sheria basi hakuna kijana atakayebaki hapa”

Hivi karibuni  Nasib Abdul ‘ Diamond Platnum’ aki mmoja wa wahanga waliofungiwa nyimbo, akihojiwa na kituo kimoja cha redio nchini alimtuhumu Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza kufungia nyimbo za wasanii zikiwamo zake  mbili za ‘Hallelujah’ na ‘Wakawaka’ bila kuzingatia hasara na usumbufu wanaoupata wakati wakiziandaa.




About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search