Waziri aagiza mhandisi akamatwe.... soma habari kamili na matukio360....#share
Na Mwandishi Wetu, Morogoro
NAIBU
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso ameagiza vyombo vya usalama kumkamata
Mhandisi Mshauri wa Kampuni ya Interconsult kutokana na kutoridhishwa na utekelezaji wa mradi wa maji wa Gombe uliopo Wilaya ya Ulanga, mkoani Morogoro.
Mhandisi Mshauri wa Kampuni ya Interconsult kutokana na kutoridhishwa na utekelezaji wa mradi wa maji wa Gombe uliopo Wilaya ya Ulanga, mkoani Morogoro.
Naibu Waziri wa Majina Umwagiliaji, Jumaa Aweso akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa ofisi ya Jumuiya yaWatumiaji Maji katika Kata yaLupiro, Wilaya ya Mahenge, mkoani Morogoro.
Pia ameagiza kufanyika uchunguzi kwenye mradi huo wa Gombe ambao umechelewa kukamilika licha ya asilimia kubwa ya fedha kuwa zimeshalipwa kwa mkandarasi, lakini pia unakosa thamani halisi ya fedha zilizotumika katika ujenzi wake.
‘‘Katika
taarifa nimeambiwa kuwa mradi unatoa maji, lakini nimekuja kuona na si kweli
wakati wizara imetoa fedh,”.
“Kama
Naibu Waziri wa Maji sitakubali kusikia fedha za miradi ya maji zinaliwa kila
ninapoenda, naagiza Mhandisi Mshauri akamatwe na uchunguzi ufanyike na endapo
itabainika amehujumu achukuliwe hatua kali ili iwe fundisho kwa wahandisi wote
nchini’’, amesema Aweso.
Amesema
kuwa wizara itaandaa orodha ya majina ya wakandarasi wote waliohujumu miradi ya
maji na kuikabidhi kwa Bodi ya Usajili ya Wakandarasi ili wafutiwe kabisa
usajili na kutopewa kazi yoyote tena nchini endapo watathibitika kufanya hivyo.
Akiwa
Ulanga Naibu Waziri Aweso amezindua ofisi ya maji ya Kata ya Lupiro, mradi wa
maji wa visima 27 katika Kijiji cha Chikuti, ambacho ni moja ya vijiji vinavyonufaika
na mradi huo na kukagua skimu ya umwagilaji ya Mnepa, iliyopo Kata ya Lupiro.
No comments:
Post a Comment