Azam FC yatupwa nje FA...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

TIMU ya Azam imeondolewa kwenye michuano ya FA na Mtibwa Sugar kwa mikwaju ya penati 9-8 kwenye mchezo wa robo fainali uliofanyika kwenye uwanja wa Azam Complex.
Mtibwa imekuwa timu ya tatu kuingia nusu fainali baada ya Stand United iliyoitoa Njombe kwa bao moja na Polisi Tanzania ikitoa Tanzania Prisons kwa mabao 2-0.

Mchezo huo ulilazimika kwenda kwenye changamoto za penati baada ya kutoka sare ya bila kufungana katika muda wa kawaida.

Azam ilicheza vizuri zaidi kipindi cha kwanza kwa kutengeneza nafasi lakini Mtibwa wao walikuwa bora kipindi cha pili huku wakionekana kujilinda kuliko kushambulia.

Penati za Mtibwa zilifungwa na Hassan Dilunga, Ismail Muhesa, Stamili Mbonde, Nditi, Hassan Isihaka, Hassan Mganga, Salum Kihimbwa, Kasian Ponera, Dickson Daud wakati Henry Joseph akikosa mkwaju wake.

Wakati zile za Azam zilifungwa na Himid Mao, Yahaya Zayd, Bruce Kangwa, Agrey Morris, Joseph Kimwaga, Joseph Mahundi, Salehe Abdallah na  Salum Abubakar wakati Frank Dumayo na Abdallah Kheri wakipoteza mikwaju.

Kesho kutakuwa na mchezo mmoja wa kukamilisha robo fainali ya michuano ambapo Singida United itaikaribisha Yanga kwenye uwanja wa Namfua.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search