Chama cha wafanyakazi serikali za mitaa cha ipongeza serikali kuwarudisha watumishi la 7 kazini...soma habari kamili na matukio360...#share
Na Abraham Ntambara,
Dar es Salaam
CHAMA cha Wafanyakazi
wa Serikali za Mitaa nchini (TALGWU) kimeipongeza serikali kwa kuwarudisha
kazini watumishi wa umma darasa la saba ambao waliokuwa wameondolewa.
Katibu Mkuu- TALGWU Rashid Mtima, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Hatua hiyo imekuja siku
moja baada ya serikali kpitia Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora George Mkuchika kutangaza kurudishwa kwa
watumishi hao na kulipwa mishahara yao ya kipindi chote ambacho walikuwa
wameondolewa.
Akitoa pongezi hizo leo
jijini Dar es Salaam akizungumza na waandhishi wa habari, Katibu Mkuu- TALGWU
Rashid Mtima amesema kwa hatua hiyo serikali imezingatia mapendekezo ya chama
chao.
“Kwa niaba ya wanachama
wote wa TALGWU nchini, napenda kutoa shukrani za dhati kwa serikali ya awamu ya
tano chini ya uongozi wa Mhe. Dokta John
Pombe Magufuli kwa kuzingatia mapendekezo yaliyowasilishwa na chama serikalini,”
amesema Mtima.
Mtima pia ametoa
shukrani kwa waziri mkuu Kassim Majaliwa, waziri wa sera, bunge, kazi, ajira,
vijana na walemavu Jenista Mhagama, Waziri wa Tamisemi Seleman Jaffo, katibu
mkuu wizara ya kazi Eric Shitindi, Tamisemi Mussa Lyombe pamoja na Utumishi Dr.
Laurean Ndumbaro, TUCTA pamoja na wabunge waliozungumzia suala hilo bungeni
katika kikao cha bunge kinachoendelea mjini Dodoma.
No comments:
Post a Comment