Chuo cha utalii chaandaa tamasha la siku ya taaluma…soma habari kamili na matukio360…#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam
CHUO Kikuu cha Taifa cha Utalii (NCT) kimeandaa tamasha la
siku ya taaluma lenye ujumbe ‘Fursa za Ajira kupitia Taaluma ya Ukarimu na
Utalii’.
Kaimu Mkurugenzi wa Mafunzo na Shughuli za Kitaalam Stephen Madenge akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam,
Kaimu Mkurugenzi wa Mafunzo na Shughuli za Kitaalam Stephen Madenge amesema
lengo la tamasha hilo ni kuufahamisha umma juu ya mafunzo na huduma zitolewazo
na chuo hicho.
“Kwa kuzingatia soko, ukuaji wa sekta ya utalii na ajira za
utalii nchini, chuo kimeandaa tamasha la siku ya taaluma hapa chuoni kampasi ya
Bustani lenye ujumbe ‘Fursa za Ajira kupitia Taaluma ya Ukarimu na Utalii’,”
amesema Madenge.
Madenge amesema kwa kutumia tamasha hilo wanafunzi wataonesha
kwa vitendo uhodari wa taaluma zinazotolewa chuoni hapo ikiwa ni pamoja na live cooking, cocktail na pastry products
making, wine testing and tents preparation.
Amesema pamoja na hayo kutakuwa na uwasilishwaji wa mada za
ukarimu na utalii kutoka kwa wataalamu mahiri wa sekta ya ukarimu na utalii wa
hapa nchini.
“Kwa ujumla tunategemea tamasha hili, liwaunganishe na
kuwaleta kwa pamoja wadau mbalimbali wa chuo kama hoteli, kampuni za kitalii,
banki, kampuni za mawasiliano, kampuni za vinywaji na chakula, vyombo vya
habari, Balozi, Taasisi, Idara na Wizara mbalimbali, wanafunzi wa shule za
sekondari, wazazi na jamii kwa ujumla,” amesema.
Mategemeo mengine ni kufahamisha umma kuhusu mafunzo na
huduma zitolewazo na chuo cha taifa cha utalii, kufahamisha umma juu ya fursa
zinazopatikana katika taaluma ya ukarimu na utalii na sekta zakwe kwa ujumla.
Pamoja na kuwaunganisha wahitimu/ wanafunzi wao, wadau hasa
waajiri wa sekta ya ukarimu na utalii na kuwaeleza wanafunzi juu ya huduma na
muendelezo wa taaluma ya ukarimu na utalii baada ya kuhitimu mafunzo yao.
Amesema kwa upande wa wadau wategemee kupata wahitimu bora
watakao wapatia ajira, kuwa karibu na jamii ambapo wanategemea kuwa na
washiriki 800 na kupata muda wa kuifahamisha jamii juu ya huduma wanazotoa
pamoja na kusambaza vipeperushi.
Hivyo amewakaribisha watu wote na wa sekta zote kushiriki
katika tamasha hilo ambapo tamasha hilo litafanyika Aprili 27, 2018.
No comments:
Post a Comment