Jebby azikwa...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Msanii wa Bongo Fleva, Jebby amezikwa katika makaburi ya Mailimbili mjini Dodoma.

Jebby ambaye amewahi kufanya vizuri na wimbo wake wa ‘Swahiba’ alifariki dunia hapo jana April 22, 2018 mjini Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabu.

Wapili kushoto ni msanii Suma G.
Kwa mujibu wa mdogo Jebby, Hamis Omary msanii huyo hakubahatika kuwa na mke wala mtoto, pia kuna nyimbo zaidi ya nne alirekodi ambazo zipo tayari ila hazijatoka.
Professor Jay ni miongoni mwa wasanii waliohudhuria katika msiba huo ambapo amekabidhi Tsh. 550,000 zilizochangwa na wasanii kwa ajili ya msiba huo, msanii mwingine aliyehudhuria ni pamoja na Suma G.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search