HakiElimu yataja changamoto saba sekta ya elimu nchini…soma habari kamili na matukio360...#share


Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

TAASISI ya HakiElimu imetaja changamoto saba zinazotakiwa kushughulikiwa na serikali kwenye mpango bajeti wa sekta ya elimu kwa mwaka wa fedha 2018/2019 ili kuiboresha sekta hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji HakiElimu Dk. John Kalage akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Changamoto hizo ni upungufu wa fedha zinazotengwa kwa ajili ya bajeti ya sekta ya elimu, upungufu wa bajeti ya maendeleo ya sekta ya elimu na kutenga fedha zinazojitosheleza, kutatua changamoto za utekelezaji wa bajeti ya maendeleo ya sekta ya elimu.

Nyingine ni kushughulikia changamoto za miundombinu mashuleni, Bajeti kwa ajili ya ajira za walimu, bajeti kwa ajili ya ruzuku kwa wanafunzi na bajeti kwa ajili ya elimu kwa mtoto wa kike.

Changamoto hizo zimetajwa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa HakiElimu Dk. John Kalage alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari wakati akitoa muhtasari wa taarifa ya taasisi hiyo kuhusu mpango wa bajeti ya sekta ya elimu kwa mwaka wa fedha 2018/2019.

“…tunatambua kuwa jitihada za serikali zinakabiliwa na changamoto mbalimbali ambazo zinafifisha ubora na kudumaza juhudi za uboreshaji wa elimu nchini. Mathalani, katika miaka ya hivi karibuni, sekta ya elimu imekabiliwa na kushuka kwa uwezo wa kusoma, kuandika na kuhesabu kwa wanafunzi wa elimu ya msingi wa madaraja yote (UWEZO, 2017) amesema Dk. Kalage.

“Ni asilimia 20 tu ya wanafunzi wa darasa la nne nchini wanauwezo wa kusoma sentensi kwa ufasaha na chini ya asilimia 10 wakiwa na uwezo wa kusoma aya kwa mujibu wa Ripoti ya Benki ya Dunia (2018), huku matokeo ya mitihani ya mwisho kidato cha pili na nne yakionesha ufaulu hafifu ambapo wastani wa asilimia 60 ya watahiniwa wanapata alama za daraja la nne na sifuri,” ameongeza.

Dk. Kalage ametoa mapendekezo yakufanywa na serikali katika bajati ya 2018/2019 ili kukabiliana na changamoto hizo na mioungoni mwa mapendekezo hayo ni serikali ielekeze asilimia 20 ya bajeti ya serikali kwenda katika sekta ya elimu ili kukidhi mahitaji ya sekta na kukazia utekelezaji wa makubaliano ya kikanda na kimataifa.

Mengine ni serikali itenge na kuongeza bajeti kwa ajili ya miradi ya maendeleo katika sekta ya elimu na hasa fedha zinazokwenda TAMISEMI kwa ajili ya elimu ya msingi. Serikali itenge bajeti yenye uhalisia wa kutatua changamoto sugu na za muda mrefu za miundombinu ambazo kwa muda mrefu zimekuwa zikiathiri mazingira ya kusoma na kufundisha katika shule za serikali.
Ameshauri serikali kuweka kipaumbele katika suala la ajira za walimu ili kutatua tatizo hilo endelevu linalosababisha changamoto kubwa za kujifunzia shuleni na kwa sababu wasichana ndiyo waathirika wakuu wa mazingira na miundombinu duni ya kujifunzia katika shule za serikali  ni muhimu masuala yanayoboresha ustawi wao kupewa kipaumbele katika bajeti ya mwaka wa fedha 2018/19.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search