Halima Mdee aachiwa kwa dhamana...soma habari kamili na matukio360...#share


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mkazi Kisutu, imemuachia kwa dhamana Mbunge wa Kawe jijini Dar es Salaam kwa tiketi ya Chadema Halima Mdee.

Hatua hiyo imekuja leo baada ya mbunge huyo kufikishwa na kuunganishwa na viongozi wenzake  wa chadema wakiongozwa na mwenyekiti wao Freeman Mbowe ambao moja ya kesi inayowakabili ni kufanya maandamano ya siyo ya halali.

Hivyo Mdee amesomewa mashtaka mawili ya kufanya mkusanyiko usio halali na kuendelea na mkusanyiko huo, kutotii amri iliyowataka kutawanyika na kusababisha vurugu iliyosababisha kifo cha Akwilina Akwilini na askari kujeruhiwa.

Baada ya kusomewa mashitaka hayo, Mahakama imempa  dhamana kwa masharti ya kuwa na wadhamini wawili watakaosaini kwa maandishi bondi ya Sh milioni 20 na kuripoti mara moja kila wiki.

Mahakama  imesema haiwezi kumnyima mshtakiwa dhamana kwa sababu aliruka dhamana ya polisi maana  polisi ni taasisi nyingine na mahakama ni taasisi nyingine, hivyo ikampatia dhamana mshtakiwa kwa masharti tajwa hapo juu.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search