Hatua ya Chadema baada ya Mdee kuwekwa mahabausu...soma habari kamili na matukio360...#share
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kumpelekea daktari wa Mbunge wa Kawe, Halima Mdee ili aweze kumcheki na kulithibitishia Jeshi la Polisi kuwa ni mgonjwa.
Hatua hiyo imekuja baada ya mbunge huyo kushikiliwa na jeshi la polisi Kanda ya Dar es Salaam mapema alfajiri ya leo akiwa Airpot alipowasili akitokea Afrika kusini kwa matibabu.
Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Itifaki na Mawasiliano ya Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema, amesema lengo ni kuthibitisha kuwa hakuwa na nia ya kukimbia kuripoti Polisi.
"Halima Mdee bado anashikiliwa na Jeshi la Polisi wa kituo cha 'Centro' Jijini Dar es Salaam mpaka hivi sasa japokuwa amewaeleza ukweli kwamba ametoka kwenye matibabu na kuwaonesha vyeti vyote vya hospitali lakini bado wanaendelea kumshikiria", amesema Mrema
Pamoja na hayo, Mrema ameendelea kwa kusema "mpaka sasa hivi hatua tulizozichukua ni kumpeleka daktari wake ili aende kumcheki na kuwathibitishia Polisi kuwa Halima kweli ni mgonjwa pia wanasheria wa chama wataelekea kituoni hapo muda si mrefu".
Halima Mdee ni miongoni mwa viongozi wa Chadema wanaotuhumiwa na Jeshi la Polisi kufanya maandamano yasiyokuwa na kibali kipindi cha uchaguzi mdogo wa marudio katika jimbo la Kinondoni
No comments:
Post a Comment