Kikwete amtakia kila la kheri Alikiba katika ndoa yake...soma habari kamili na matukio360...#share

RAIS Mstaafu wa awamu ya nne Dk. Jakaya Mrisho Kikwete amemshukuru msanii wa muziki wa kizazi kipya Ali Kiba kwa kumtembelea nyumbani kwake  na kusema kuwa amempa taarifa kuwa ataoa hivi karibuni.
Kikwete amesema hayo jana kupitia ukurasa  wake wa twitter na kusema kuwa msanii huyo ambaye sasa bado anafanya vyema na wimbo wake wa 'Seduce me' amemwambia anatarajia kuoa siku za karibuni.

"Namshukuru Alikiba kuja kunitembelea na kunitaarifu kuwa anatarajia kuoa hivi karibuni. Nimempatia nasaha zangu na kumtakia kila la kheri kwa jambo hilo jema aliloamua kufanya"alisema Kikwete 


Advertisement

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search