Mhagama ataka wanaoratibu maandamano kufuata sheria...soma habari kamili na matukio360...#share
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana,
Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama ametoa ushauri kuhusu suala la maandamano na
kusema kuwa mtu yoyote ambaye anaratibu maandamano lazima afuate sheria hata
kama maandamano yanatambulika kikatiba.
Jenista Mhagama
Amesema hayo bungeni na kudai kama kila mtu ataamua kuandamana
kwa kuwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaruhusu hilo litakuwa
jambo ambalo si sawa hivyo amevitaka vyama vya siasa kufuata sheria za nchi na
si kuvunja sheria za nchi.
"Suala la maandamano katika nchi yetu ya Tanzania
linaratibiwa na sheria za usalama ndani ya nchi chini ya vyombo vya usalama
hasa polisi na Katiba haiwezi kuchukuliwa kwamba ni kigezo cha kuviruhusu vyama
kufanya maandamano bila kuzingatia taratibu na sheria zilizowekwa.
"Ninaomba sana Watanzania wote na niviombe vyama vyote vya
siasa katika nchi yetu ya Tanzania wahakikishe wanazingatia sheria.
"Katiba yetu imeruhusu maandamano lakini maandamano
yameratibiwa kisheria na kama yameratibiwa kisheria lazima tuhakikishe kwamba
tunazingatia sheria katika kuratibu maandamano nchini kwetu Tanzania"
Jenista Mhagama aliendelea kutoa maelezo kuhusu masuala ya
maandamano
"Labda niulize swali moja tukiamka hapa siku moja asubuhi
na kila mtu ameamua kuandamana wakulima, wafanyakazi yaani kila mtu aamue tu
kuandamana kwa sababu tu Katiba imesema nadhani itakuwa siyo sawa na nichukue
nafasi hii kuviomba vyama vya siasa kuheshimu Katiba na sheria katika
kutekeleza wajibu wao na siyo kuvunja sheria za nchi yetu Tanzania"
No comments:
Post a Comment