Mjema azindua ujenzi soko jipya Kisutu...soma habari kamili na matukio360...#share


Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

MKUU wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema  amezindua ujenzi wa soko jipya la kisasa la Kisutu, jijini Dar es Salaam ambao unatarajia kukamilika ndani ya kipindi cha miezi 18.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema (kushoto) na viongozi wa soko la Kisutu jijini Dar es Salaam, wakiwa wameshika ramani ya soko la kisasa linalotarajiwa kujengwa.

Akizungumza leo na wafanyabiashara wa Kisutu wakati wa uzinduzi huo, Mjema amesema soko hilo litagharimu sh.bilioni 16 ambapo kwa sasa tayari serikali imekwishawapatia sh.bilioni mbili kwa ajili ya kuanza kwa ujenzi huo wa jengo la ghorofa nne.

“Taratibu zimekwishakamilika na tumeshampata mkandarasi, hivyo tutahakikisha mkandarasi anajenga kwa ubora viwango na kwa muda tuliokubaliana au ikibidi chini ya muda huo,” amesema Mjema.

Mjema amesema wakati wa ujenzi wafanyabiashara wa katika soko hilo wataondolewa na kupelekwa maeneo mengine yaliyotengwa kupisha shughuli hiyo ambapo amewahakikishia kuwa pindi utakapokamilika watapewa kipaumbele katika kufanyabiashara.

Amesema Soko hilo likishakamilika litakuwa miongoni mwa masoko bora mkoani Dar es Salaam .

"Soko hili likikamilika litakuwa miongoni mwa masoko bora na la mfano,” amesema .

Aidha, mkuu huyo amewataka wafanyabiasha walikuwepo sokoni hapo ambao wanapisha ujenzi wa soko kutoa ushirikiano katika ujenzi ikiwemo kuondoka katika eneo ilo na kwenda kwenye maeneo waliopangiwa na Halmashauri.

“Tunawaomba wafanyabiasha ninyi 633 mtoe ushirikiano katika ujenzi ,Muende kwenye maeneo mliotengewa kwa Muda kwani Halmashauri imetenga milioni 138 za kwenda kukarabati soko la mda la pale kisuto ambao watakwenda wafanyabiashara za mboga,” ameongeza.

Ameleza kuwa wafanyabiashara wa nyama ya kuku wametakiwa kwenda kufanyia biashara  Mkunguni huku wafanyabiashara wa mboga mboga na matunda wao wakiendelea kufanyia Kisutu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ilala, Msongela Palela  amesema ujenzi wa soko hilo ni wa Gorofa nne.

Amesema kuwa  litakapokamilika litakuwa maeneo ya kufanyia biashara, kupaki magari, kutakuwa na maeneo maalum ya Benki.
Aliyesimama ni Mkurugenzi wa halmashauri ya manispaa ya Ilala Msongela Palela, akizungumza wakati wa uzinduzi wa soko jipya la kisasa la Kisutu jijini Dar es Salaam.

Mkuu wa wilaya ya Ilala Sophia Mjema akizungumza na wafanyabiashara wa soko la Kisutu jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi huo.
Mkuu wa wilaya ya Ilala Sophia Mjema na wafanyabiashara wanawake wa soko la Kisutu jijini Dar es Salaam wakiwa wameshika ramani ya soko linalotarajiwa kujengwa.
Ni sehemu ya wafanyabiashara wa soko la Kisutu jijini Dar es Salaam waliohudhuria katika uzinduzi wa soko jipya la kisasa la Kisutu.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search