IGP Sirro "feki' atiwa mbaroni...soma habari kamili na matukio360...#share


Na Mwandishi Wetu, Njombe

MTU mmoja aliyetambulika kwa jina la Maricha Mniko(30) Mkurya dereva na mkazi wa Tandala Wilayani Makete anashikiliwa na jeshi la polisi Mkoani Njombe kwa tuhuma za kujifanya ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro ili kumsaidia ndugu yake kupata kazi katika kampuni ya magari ya Japanisee.

Hayo yamesemwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Renata Mziga ambapo amesema kuwa tukio hilo limetokea Mei 18 mwaka huu ambapo mtuhumiwa anadaiwa kumpigia simu Daniel Junishi mmiliki wa kampuni ya magari ya Japanisee.

Kamanda Mziga amesema kuwa baada ya kumpigia mtuhumiwa huyo inadaiwa alijitambulisha kuwa ni mkuu wa jeshi la polisi nchini hivyo anatakiwa amwajili mdogo wake aliyeko mkoa wa Mara.

“Baada ya kumwambia huyu mmiliki wa magari ya Japanisee alimuuliza kuwa namba yangu umeipata wapi akajibu nimepewa na Kamanda wa Polisi Mkoa Njombe na akasema yupo Dodoma,”amesema Kamanda Mziga.

Aidha, Kamanda Mziga ametoa rai kwa wananchi Mkoani humo kuwafichua watu wanaopiga simu kwa kutumia majina ya viongozi kwa maslahi yao binafsi.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search