Mwijage awekwa kikaangoni Bungeni...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Akiwa katika maandalizi ya kujibu swali hilo Mh. Mwijage amesema kwamba sababu ya sukari Tanzania bara kuuzwa ghali sana ni kutokana na gharama za uzalishaji bara kuwa juu sana kuliko Zanzibar jibu ambalo lilizua kelele nyingi za Wabunge.
"Mh. Spika nimejitahidi sana kuelezea suala hili lakini muda hautoshi....... Gharama za uzalishaji sukari bara zipo juu kuliko Zanzibar. Nimepewa muda naomba muache niwaeleze....Hili suala siyo rahisi kama mnavyofikiria.... Ndiyo siyo suala rahisi naomba niwaeleze," Mwijage akifafanua huku wabunge wakizidi kupiga kelele.
"I am very good in talking, I can talk....... Mh. Turky ulipopewa kibali na serikali kuingiza sukari ni kwa nini wewe hukuuza rahisi?"Ameongeza Mwijage.
Awali katika swali lake Mh. Turky alitaka kujua kwa nini viwanda vya Tanzania Bara vimekuwa vikishindwa kushusha bei za sukari ilhali Viwanda vya Zanzibar vinauza sukar sh 65000.
Akitolea mfano soko la dunia amesema kwamba "Sukari inauzwa dola 390 ukilipia kodi 25% na VAT 18% sukari inasimama kwa bei ya sh 65000. Watanzania wanalanguliwa kwa kuuziwa sukari 110000 kwa misingi gani"?
Pamoja na hayo Mbunge huyo amesema kwamba "Tulishaomba Cost of Production (Gharama za uzalishaji) hapa bungeni tangu Naibu Waziri akiwa Malima na hatujaweza kuletewa mpaka leo"
No comments:
Post a Comment