TIC yaandikisha miradi ya Dolla za Kimarekeni milioni 13 kwa miezi minne...soma habari kamili na matukio360...#share
Na Abraham Ntambara,
Dar es Salaam
KITUO cha Uwekezaji nchini (TIC) kimesema kwa kipindi cha miezi minne
kimeweza kuandikisha miradi mipya 109 ambayo inatarajiwa kuwekeza kiasi cha
Dolla za Kimarekani zaidi ya milioni 13.
Mkurugenzi Mtendaji wa TIC Geoffrey Mwambe akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Hayo yamebainishwa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi
Mtendaji wa kituo hicho Geoffrey Mwambe alipokuwa akizungumza na waandishi wa
habari juu ya baadhi ya mafanikio ya TIC, amesema inatarajia kuajiri
wafanyakazi wapya 18,172.
“Uwekezaji zaidi umefanyika katika sekta za ujenzi, uzalishaji
viwanda, usafirishaji, kilimo na miundombinu,” amesema Mwambe.
Mwambe amebainisha kuwa katika miradi hiyo 28 sawa na asilimia
34.86 inamilikiwa na wageni, miradi mitatu sawa na asilimia 2.75 ni ya ubia na
miradi 68 sawa na 62.40 inamilikiwa na Watanzania.
Aidha amesema uchambuzi huo
unaonesha kuwepo kwa mwamko mkubwa kwa wawekezaji wazawa katika sekta za
viwanda, kilimo na miundombinu tofauti na ilivyozoeleka ambapo uwekezaji
ulijikita katika sekta za utalii na usafirishaji wa mizigo.
Amewataka wakuu wa mikoa pamoja na wakuu wa wilaya na taasisi
mbalimbali za kiserikali kukuza mazingira wezeshi ya uwekezaji ikiwemo kutenga
maeneo ya kuwekeza.
Amesisitiza wakuu hao
wa mikoa , kufanya tasmini ya mara kwa mara ya kuhusiana na uwekezaji katika
mikoa yao, ambapo amewataka kutowanyanyasa wawekezaji na kuboresha mazingira
wezeshi kwa wafanyabiasha.
Amesema kuwa juhudi hizo zikfanyika kwa nguvu na msisitizo mkubwa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa
sekta hiyo, kutawezesha kukuza uwekezaji nchini na kuibua fursa kubwa za ajira
kwa vijana.
Ameeleza kwamba kama taasisi mbalimbali zitaweka jitihada kubwa katika kuwekeza kwenye sekta ya
viwanda kutasaidia kupanua wigo wa walipa kodi, na hatimaye kuongeza uzalishaji
na kufikia uchumi wa kati.
Amezitaka taasisi zote nchini
pamoja na mamlaka zote husika kukuza ushirikiano na kituo hicho cha uwekezaji ili
kuweza kujenga uelewa na kutoa miongozo kwa ajili ya kuweza kusimamia ujenzi wa
viwanda nchini.
Mkurugenzi huyo amesema kuwa kituo chake kimeongeza
ofisi nne mpya za kanda katika mikoa ya Dodoma, Dar es salaam, Mtwara na kigoma
ambazo ni kanda ya kati, wakati kanda ya mashariki vituo vilivyoongezwa ni
pamoja na pwani na Dar es salaam.
"Uboreshaji wa huduma
katika kituo cha uwekezaji unasaidiwa zaidi na mfumo uitwao (one stop
facilitation Center) ndani ya ofisi zetu ambapo mfumo huo hutoa huduma za
usajili wa makampuni pamoja na kodi" amwsema Mwambe.
Hata hivyo kituo hicho
kinashirikiana na Serikali katika kutoa ushauri na kuboresha mazingira ya
uwekezaji ambapo kulingana na Takwimu za Benki ya Rand Merchant (RMB)
zilizotolewa mwaka 2015, Tanzania ilishika nafasi ya Tisa kati ya nchi kumi
zenye ushawishi wa kuvutia waweze kuwekeza.
No comments:
Post a Comment