Wadau waunga mkono baadhi vipegele kanuni za maudhui ya mitandao...soma habari kamili na matukio360..#share

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

BAADHI ya wadau wameunga mkono baadhi ya vipengele katika kanuni  za maudhui ya mitandao vyenye kulinda maadili na utu.




Mmoja wa wa wadau wa mitandao ya kijamii  akizungumza kuhusu mitandao ya kijamii inavyoweza kukuza utawala bora.

Hayo  yanakuja wakati huu ambao kumekuwa na malalamiko juu ya kanuni hizo mpya za maudhui ya mitandao ambazo zimetolewa hivi karibuni na serikali kwani zinadaiwa kuminya uhuru wa kujieleza.

Baadhi ya vipengele vinavyoungwa mkono vinahusu kulinda haki za mtoto, kuzuia matusi mtandaoni na hata kupunguza picha zisizofaa.

Hayo yamebainishwa leo jijini Dar es Salaam na wadau mbalimbali wakati wakichangia mdahalo ulioandaliwa na Kituo cha Sheria na Haki za binadamu (LHRC) uliokuwa na lengo la kujadili mchango wa mitandao ya kijamii katika kukuza utawala bora.




Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Jamii Forums, Maxence Melo, Mkurugenzi wa Utetezi na Maboresho Kituo Cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Anna Henga (katikati) na Mwanasheria wa LHRC, William Kahale wakiwa katika mdahalo  huo.
Washiriki wa mdahalo huo wakifuatilia kilichokuwa kikiendelea.



Baadhi ya watoa mada wa mdahalo  walivyoonekana meza kuu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search