MAGUFULI AWAPA ULAJI MADAKTARI 500, KWENDA KENYA KUFANYAKAZI KWA MKATABA MAALUM!!



WIZARA YAWEKA HADHARANI; WENYE VIGEZO WATAKIWA KUOMBA...

Kutoka na mgomo wa madaktari nchini Kenya,  Rais Uhuru Kenyata ameiomba Serikali ya Tanzania kumsaidia Madaktari ambao wanafanya chini ya mkataba wa miaka mawili nchini huko.

Kutokana na ombi hilo,Serikali Tanzania inatarajia kupeleka madaktari 500 nchini Kenya ifikapo Aprili mwaka huu, ikiwa ni kukubali ombi la Rais Uhuru Kenyatta.

Madaktari hao watakaopatiwa ajira ya mkataba wa miaka miwili, ni wale ambao hawapo katika mfumo wowote wa ajira serikalini lakini wenye vigezo stahiki.

Akizungumza kwenye mkutano na vyombo vya habari leo, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu alisema Rais John Magufuli amepokea ombi hilo huku akiwataka wenye vigezo kuhakikisha wanatuma maombi yao kabla ya Machi  27.

"Daktari anatakiwa asiwe ameajiriwa katika hospitali ya Umma, awe amepata mafunzo kwa vitendo na pia awe amesajiliwa na Baraza la Madaktari Tanzania," alisema Ummy Mwalimu.

Source: tanzaniampyamatukio blog

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search