MAKALA: AFYA YA JAMII - MADHARA YANAYOSABABISHWA NA ULAJI MWINGI WA SUKARI
PITIA MAKALA HII YA UCHAMBUZI UWEZE KUZIJUA NJIA NNE (4) KUU ZA KUPUNGUZA ULAJI MWINGI WA SUKARI
Tunafahamu kuwa ulaji wa sukari kupita kiasi unahusishwa na kuongezeka
kwa unene, uzito kupita kiasi, ugonjwa wa kisukari cha ukubwani (aina ya pili),
magonjwa ya moyo, baadhi ya saratani, kuoza kwa meno na ugonjwa wa ini.
![]() |
| Mfumo wa mwili wa binadamu unaothiriwa na ulaji mwingi wa sukari! |
Hata hivyo katika nchi zinazoendelea kama Tanzania, siyo rahisi kufanya
tafiti zinazoonyesha kiasi cha sukari anacho kula mtu kwa siku.
Lakini baadhi ya tafiti za miaka ya 2008-2009 zinaonyesha kuwa nchini ya
Marekani mtu mzima kwa wastani anakula sukari vijiko vya chai 22 kutoka katika
vyakula vilivyosindikwa kiwandani.
Kwa mujibu wa Taasisi ya Kimarekani ya Mambo ya Moyo (Aha), kwa watu
wazima, wanawake, matumizi yao ya sukari inayotokana na vyakula vilivyosindikwa
kiwandani, yasizidi vijiko sita vya chai kwa siku.
Huku kwa upande wa wanaume wasizidishe vijiko tisa kwa siku na kwamba
wataalamu wanabainisha kuwa kila gramu nne za sukari ni sawa na sukari iliyojaa
katika kijiko kimoja cha chai.
Wataalamu hao wanasisistiza kuwa maelezo katika vyakula vilivyosindikwa
viwandani yawe kwenye kifungashio cha bidhaa.
Sukari ni chanzo muhimu cha nishati mwilini.
Watu wanasema bila sukari hakuna uhai, hivyo kuacha
kabisa kula vyakula vya wanga na vyenye sukari unaweza kusababisha mwili kuwa
na kiwango kidogo sana cha sukari na kuathiri ufanyaji kazi wa ubongo na viungo
vingine.
Na kwamba hali kama hiyo ikiendelea, mtu anaweza
kuishiwa nguvu na kupoteza fahamu na wakati mwingine kusababisha kifo kwani
sukari nyingi ni sumu na inadhuru afya.
Ulaji wa sukari kupita kiasi unahusishwa na
kuongezeka kwa unene, uzito kupita kiasi, ugonjwa wa kisukari cha ukubwani
(aina ya pili), magonjwa ya moyo, baadhi ya saratani, kuoza kwa meno na ugonjwa
wa ini.
Njia 4 kuu za kupunguza ulaji wa sukari:
Miongoni mwa njia hizo ni kwanza ni:
·
kuwa na ufahamu wa kutosha kuhusu
hatari ya kiafya inayotokana na ulaji wa sukari nyingi. Matumizi hayo ya sukari yanamfanya mtu awe anapenda sukari mfano kwa
wale walio athiriwa na dawa za kulevya.
·
Njia ya pili ni kubainisha chanzo
kikubwa cha sukari katika vyakula na vinywaji unavyotumia kila siku, hapa
unatakiwa kupunguza unywaji wa juisi za viwandani na vitu vingine ambavyo ni
vitamu.
·
Vile vile, jambo jingine ni kupunguza
matumizi ya ulaji wa vyakula vyenye sukari kama vile chai yenye sukari nyingi,
keki, mikate ya kumimina au visheti.
![]() |
Tende: ni moja chakula mbadala vinavyosaidia kupunguza ongezeko la sukari nying mwilini |
Unaweza
chunguza pia kama una kawaida ya kula vyakula vyenye kiwango kikubwa cha sukari
ama wanga. Mfano kilichotokana na unga wa mahindi yaliyokobolewa.
Baada
ya kujua chanzo kikuu, weka mpango wa kupunguza ulaji wa vyakula hivyo.
·
Kama unaweka vijiko vinne vya sukari
katika chai au kahawa, punguza hatua kila wiki kijiko kimoja na hiyo itapunguza
tatizo hilo.
Hata hivyo baada ya wiki tatu utakuwa unakunywa chai na kuweka kijiko
kimoja cha sukari.
Hivyo kama unakunywa soda kila siku chupa tatu, asubuhi, mchana na jioni
sasa unashauriwa kupunguza iwe chupa moja kila siku na baada ya wiki moja
punguza mpaka uweze kunywa chupa moja ya soda kila baada ya siku mbili na
baadaye uweze kunywa soda chupa mbili kwa wiki.
![]() |
Sukari ya viwandani |
Baada ya hapo unaweza kujitathimini sasa kama unaweza kuishia hapo au
kuacha kabisa kunywa vinywaji hivyo na kutumia vinywaji halisi kwa kusaga
matunda bila kuweka sukari.
Mwisho.






No comments:
Post a Comment