RAIS MAGUFULI AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA BANDARI YA DAR ES SALAAM, ABAINI 'UOZO' WA KUTISHA!!

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 23 Machi, 2017 amefanya ziara ya kushtukiza katika bandari ya Dar es Salaam kwa lengo la kufuatilia utekelezaji wa maelekezo aliyoyatoa kwa nyakati tofauti juu ya kudhibiti udanganyifu wa mizigo inayoingia na kutoka nchini kupitia bandari hiyo ikiwemo usafirishaji wa mchanga wa madini kwenda nje ya nchi.


Katika ziara hiyo Mhe. Rais Magufuli ameshuhudia makontena 20 ya mchanga wenye madini kutoka kwenye migodi iliyopo kanda ya ziwa ambayo yamezuiliwa kusafirishwa nje ya nchi tangu alipotoa agizo la kupiga marufuku usafirishaji wa mchanga nje ya nchi tarehe 02 Machi, 2017........

Tanzania mpya: imekuwekea ujionee mwenyewe yaliyojiri jana wakati wa ziara hiyo ya mhe. Rais....



Mhe. Rais akiongea mara baada ya kujionea 'madudu' wakati wa ziara yake katika bandari ya dar es Salaam jana.

17498471_10208672062378177_2303612127545512557_n.jpg
Mhe. Rais Dkt. Makufuli akionyeshwa moja ya makontena yaliyodaiwa kufanyiwa udanganyifu.


17309816_10208672062578182_5022295759993761281_n.jpg
Rais Magufuli akiendelea na ukaguzi wake katika kitengo cha makontena kufuatia ziara yake ya kushtukiza aliyoifanya bandarini jana.


Source: Taarifa ya Ikulu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search