BREAKING NEWS!! MUHIMBILI WAENDESHA UPASUAJI WA KIHISTORIA
![]() |
| Mojawapo ya Majengo makuu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili |
Hospitali ya Taifa Muhimbili leo imeanza kufanya upasuaji wa kihistoria wa kuondoa uvimbe 'fibroid' kwa wanawake ambao umefanyika kwa njia ya matundu madogo (laparoscopic Surgery).
Upasuaji huo unaofanyika katika chumba kikuu cha upasuaji, unaenda sambamba na mafunzo kwa vitendo kwa madaktari zaidi ya 30 ambao wanafuatilia moja kwa moja kwa njia ya runinga wakiwa chumba cha mkutano. Daktari bingwa wa uzazi na magonjwa ya wanawake Vicent Tarimo alisema upasuaji wa aina hiyo kwa njia ya kawaida huchukua takribani saa moja na nusu mpaka mawili, lakini kwa njia hiyo ya kisasa wamefanikiwa kumtibu mwanamke aliyekuwa na uvimbe kwenye mirija ya uzazi kwa saa moja.
"Zaidi ya wanawake 15 watanufaika na upasuaji huu na wengi wamekuwa na tatizo la uvimbe sehemu mbalimbali kuzunguka kizazi," alisema.




No comments:
Post a Comment