HAJI MANARA AFUNGUKA MAZITO YA HUKUMU YA TFF.. ASEMA ATAPAMBANIA HAKI KWA VIWANGO VYA JUU !!


MSEMAJI MKUU wa Simba aliyefungiwa, Haji Sunday Manara amefunguka mazito kuhusu hukumu iliyotolewa dhidi yake akidai kwamba hakutendewa haki.
Akiongea kupitia ukurasa wake wa Instagram baada ya kurejea kutoka katika majukumu ya kifamilia Zanzibar ameelezea mkasa mzima na kwamba hakuona uharaka wa TFF kung’ang’ania kutoa maamuzi licha ya mwajiri wake kuiandikia barua TFF ya kuomba kusogeza mbele kikao mpaka siku ya J’nne ili apewe nafasi ya kusikilizwa.
“Mimi si mtu ninayeamini uonevu na si mtu ninayeweza kunyamaza nikiona haki inaporwa…” alisema Haji.
Akielezea kadhia nzima ya maamuzi ya TFF Haji alisema…
Mimi si mtu mwenye moyo dhaifu wa kuogopa kukosoa pale panapopaswa kurekebishwa, na always nitabaki hivyo…”,
Haji amesema kuwa siku alipopata taarifa ya kuitwa TFF,  alikuwa Zanzibar kwa maswala ya kifamilia na ndipo mwajiri wake alivyoandika barua kuomba kusogezwa mbele kwa kikao hicho jambo ambalo TFF ilipuuzia.
“Barua iliwafikia na binafsi nikaongea na Afred Lucas msemaji wao na akanijibu ameipokea yeye na imegongwa muhuri na Katibu Mkuu wa TFF ameshaipata”
Ni uharaka upi iliyonao TFF wa kushindwa kunipa nafasi ya kunisikiliza?, alisema Haji na kuongeza… Natural justice nchi hii haitambuliki,.. endapo wahaini na wauaji hupewa nafasi ya kusikilizwa iweje kwangu ninaepiga kelele kutetea haki ya mwajiri wangu ? aliuliza Haji.

“Nimejiuliza, hivi ni kaka yangu huyu Msemwa aliyesoma hii hukumu?...  ukweli ni kwamba nimemuona kwa Millard Ayo, anasoma hukumu iliyo kinyume cha hati ya mashtaka,…”
“Ni aina ya hukumu katili zaidi kwa viwango vya mpira wetu, ila nawaambia TFF Haji hajawahi kuwa dhaifu wa moyo, anaweza kuwa dhaifu wa kiwiliwili, lakini nina moyo wa Simba,… nitapambana kutetea haki yangu na ya mwajiri wangu kwa viwango... alimaliza.

Je, Haji kaonewa au hajaonewa?… tupe maoni yako. 

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search