MH. WAZIRI ANGELA KAIRUKI: KIPIMO CHA VIONGOZI WA KISIASA NI KUJUA KUSOMA NA KUANDIKA HIVYO HIVYO HAWAKUHUSIKA NA ZOEZI HILI LA UHAKIKI WA KUBAINI VYETI FEKI !




Akiwasilisha taarifu fupi ya zoezi la uhakiki waziri Kairuki alikuwa na haya ya kusema: 

"Zoezi hili la uhakiki lilihusisha watumishi wa umma pekee wakiwemo Makatibu wakuu na watendaji wengine. Watumishi hawa wanatakiwa kuwa na sifa za kutumikia nafasi zao.

Zoezi hili halikuhusisha Viongozi wa Kisiasa wakiwemo Mawaziri, Wabunge, Wakuu wa Mikoa/Wilaya na Madiwani ambao wanatakiwa kujua kusoma na kuandika tu!

Ripoti hii inaonesha kuwa tayari watumishi wa Umma 400035 wamehakikiwa.

Matokeo ya uhakiki yamegawanyika kwenye makundi manne:

1. 376969 sawa na 94.23% wana vyeti halali. Baraza limehakikisha kuwa magamba ya vyeti vilivyohakikiwa vilitolewa na NECTA na taarifa zao zinaendana na zilizopo kwenye vyeti.

2. 9932 sawa na 2.4% wamebainika kuwa na vyeti vya kughushi. Vyeti vyao havifanani na vinavyotolewa na NECTA.

3. Vyeti 1538 vinatumika na zaidi ya mtumishi mmoja ambayo ni sawa na 0.3% ya vyeti vilivyohakikiwa. Hawa tunasema wana vyeti vyenye utata.

4. 11569 waliwasilisha vyeti pungufu. Hawa waliambatanisha vyeti vya utaalamu kama udaktari au ualimu pekee bila vyeti vya kidato cha nne wala cha sita.

Kwa mujibu wa kanuni ya adhabu, adhabu ya mtu aliyefanya kosa la kughushi cheti ni kifungo Jela miaka 7.

Waziri Kairuki amekabidhi ripoti na boksi lenye majina ya watumishi na taarifa zao kamili kama wako wapi na wanapatikana wapi.


Rais anatoa kitabu na kusoma jina la mtumishi mmoja " Abdallah Chanja" na kusema mengine atayasoma kwa wakati wake.

Source: JF

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search