MACHACHE ALIYOYASEMA WAZIRI #NDALICHAKO WAKATI MHE. RAIS AKIPOKEA RIPOTI YA UHAKIKI WA VYETI FEKI !

Waziri Ndalichako

fuatana na mhe. waziri hapa....

Natoa shukrani za dhati kwa shuguli hii kufanyika Chuo kikuu Dodoma. Zipo taasisi nyingi ambazo shughuli hii ingeweza kufanyika. Wanafunzi, walimu wa Chuo wamefurahi sana ujio wako UDOM.

Ni heshima kubwa sana kwa Chuo kikuu cha UDOM.Pamoja na kuwa utapokea ripoti ya uhakiki wa vyeti pia utafungua shughuli za sherehe za miaka 10 za chuo cha UDOM

Katika wizara yangu kuna changamoto kuhusu suala la kughushi vyeti. Mwaka 2008 tulianzisha mfumo wa kuweka picha kwenye vyeti vya kitaaluma...

Kutokana na dhamira yako ya dhati Mh. Rais uliagiza watumishi wa Umma wafanyiwe uhakiki. Nashuruku mh. Kairuki aliweza kulisimamia vyema suala hili. Tunakupongeza Rais kwa kufanya maamuzi kwa vitendo.

Serikali imeziba njia zote za mkato! Wanafunzi someni, hakuna tena njia za mkato katika elimu wala ajira.

Uhakiki wa vyeti umefanyika kwa awamu tatu

1. Watumishi wa Mamlaka ya serikali za mitaa
2. Watumishi wa Taasisi na mashirika ya umma
3. Watumishi wa serikali kuu

Rais, Wizara yangu imehakiki vyeti vya kidato cha nne, sita na vyeti vya ualimu kwa watumishi wa umma.

Zoezi la uhakiki kwa awamu ya kwanza na pili umekamilika na tulikabidhi.

Uhakiki wa Vyeti vya Watumishi wa Serikali Kuu upo katika hatua za mwisho na utakabidhiwa hivi karibuni.

Napenda kuwaasa wanafunzi wa vyuo vikuu, waliojiunga vyuo vikuu either kwa kughushi au udanganyifu ni bora ukajisalimisha maana unaweza ukamaliza chuo lakini mbeleni ukakamatwa kwa vyeti feki. Majuto ni mjukuu.


Nawashukuru sana wote kwa kunisikiliza.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search