MACHACHE ALIYOYASEMA WAZIRI #NDALICHAKO WAKATI MHE. RAIS AKIPOKEA RIPOTI YA UHAKIKI WA VYETI FEKI !
![]() |
Waziri Ndalichako |
fuatana na mhe. waziri hapa....
Natoa shukrani za dhati kwa shuguli hii kufanyika Chuo
kikuu Dodoma. Zipo taasisi nyingi ambazo shughuli hii ingeweza kufanyika.
Wanafunzi, walimu wa Chuo wamefurahi sana ujio wako UDOM.
Ni heshima kubwa sana kwa Chuo kikuu cha UDOM.Pamoja
na kuwa utapokea ripoti ya uhakiki wa vyeti pia utafungua shughuli za sherehe
za miaka 10 za chuo cha UDOM
Katika wizara yangu kuna changamoto kuhusu suala la
kughushi vyeti. Mwaka 2008 tulianzisha mfumo wa kuweka picha kwenye vyeti vya
kitaaluma...
Kutokana na dhamira yako ya dhati Mh. Rais uliagiza
watumishi wa Umma wafanyiwe uhakiki. Nashuruku mh. Kairuki aliweza kulisimamia
vyema suala hili. Tunakupongeza Rais kwa kufanya maamuzi kwa vitendo.
Serikali imeziba njia zote za mkato! Wanafunzi someni,
hakuna tena njia za mkato katika elimu wala ajira.
Uhakiki wa vyeti umefanyika kwa awamu tatu
1. Watumishi wa Mamlaka ya serikali za mitaa
2. Watumishi wa Taasisi na mashirika ya umma
3. Watumishi wa serikali kuu
Rais, Wizara yangu imehakiki vyeti vya kidato cha nne,
sita na vyeti vya ualimu kwa watumishi wa umma.
Zoezi la uhakiki kwa awamu ya kwanza na pili
umekamilika na tulikabidhi.
Uhakiki wa Vyeti vya Watumishi wa Serikali Kuu upo
katika hatua za mwisho na utakabidhiwa hivi karibuni.
Napenda kuwaasa wanafunzi wa vyuo vikuu, waliojiunga
vyuo vikuu either kwa kughushi au udanganyifu ni bora ukajisalimisha maana
unaweza ukamaliza chuo lakini mbeleni ukakamatwa kwa vyeti feki. Majuto ni
mjukuu.
Nawashukuru sana wote kwa kunisikiliza.
No comments:
Post a Comment