#OLE SABAYA AACHIWA HURU !

MAHAKAMA
ya Hakimu Mkazi Arusha, leo imemuachia huru aliyekuwa Mwenyekiti wa Umoja wa
Vijana (UVCCM) Lengai Ole Sabaya baada ya kuona upande wa Jamuhuri wazembe wa
kushindwa kuleta mashahidi katika kesi ya kujifanya Afisa Usalama wa Taifa
(TISS).
Akisoma
uamuzi wake jana uliotokana na ombi la Wakili wa Serikali Grace Madikenya la
kuomba Mahakama hiyo kuiondoa kesi hiyo kwa sababu ya kukosa shahidi muhimu
katika kesi hiyo na kupingwa na Upande wa Utetezi kuwa wanatumia vibaya
mahakama kumtesa mteja wao, Gwantwa
Mwakuga,
alisema Mahakama inasikitika kuona mwendesha mashitaka wa serikali, anatumia
kigezo cha kuondoa kesi na kumkamata mshitakiwa kwa maslahi yake mwenyewe.
credit: habari za jamii
No comments:
Post a Comment