CONFIRMED: ROMA MKATOLIKI NA WENAZAKE WOTE WAMEPATIKANA!


Saa chache baada ya Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro kuwaambia waandishi wa habari kuwa hawezi kusema ni lini mwanamuziki  Roma na wenzake watapatikana, taarifa kutoka kwa mmiliki wa studio walipokamatiwa, amethibitisha kuwa wamepatikana.
J Murder ambaye ndiye mmiliki wa Tongwe Records walipokuwa Roma na wenzake kabla ya kukamatwa na watu wasiojulikana, amesema kuwa wasanii hao wamepatikana na wapo katika Kituo cha Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Hakuna taarifa yoyote iliyoeleza wasanii hao wamepatikana wapi au ni nani aliyekuwa anawashikilia na sababu hasa za kufanya hivyo ni zipi.
Roma na wenzake watatu walikamatwa na watu wasiofahamika usiku wa kuamkia Jumatano ambapo mbali na wao kuchukuliwa, watu hao pia walichukua baadhi ya vifaa vinavyotumika studio bila kueleza sababu za kufanya hivyo.

Msanii Roma Mkatoliki anadaiwa kupatikana na yupo Kituo cha Polisi Oysterbay jijini Dar.

Habari ya akina Roma kupatikana imethibitishwa na Mkurugenzi wa Tongwe Records J. Mada.

Taarifa zaidi zinafuata..(source: JF)



ROMAA.png

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search