ZUMA AKWEPA SHINIKIZO LA KUTAKA AJIUZULU

Zuma aponea shinikizo za kumtaka ajiuzulu
Kitengo hicho kilikua kinatathmini malalamiko kutoka kwa maafisa wa vyeo vya juu wa ANC, kuwa Jacob Zuma hakuwaomba ushauri wao wakatia wa mabadiliko kwenye baraza la mawaziri.
Baada ya kuyatathmini malalamiko hayo, ANC imeamu kuwa haitashinikiza kujiuzulu kwa bwana Zuma, kwa mujibu wa maafisa wa chama.
Bwana Zuma amekuwa akikumbwa na shinikizo kali tangu amfute kazi waziri wa fedha aliyekuwa akiheshimiwa Pravin Gordhan.
Bwana Gordhan alifutwa kazi kama sehemu ya mabadiliko makubwa katika baraza la mawaziri ambayo yalisababisha maswali kutoka kwa uongozi wa ANC ikiwa Zuma atasalia kuwa rais.
Washirika wakubwa wa ANC kikiwemo chama cha SACP na cha Cosatu, walijiunga katika wito wa kumtaka Zuma ajiuzuku.
Lakini kamati iliyokuwa ikijadili suala la mabadiliko ya baraza la mawaziri ya NWC imemuunga mkono Zuma.
Kamati ya NWC ndiyo ya pili kwa utoaji wa maamuzi katika chama cha ANC.
SOURCE: BBC SWAHILI

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search