MANISPAA YA UBUNGO YAFANYA OPERESHENI MAALUM YA UKUSANYAJI MAPATO MANZESE

Kamati ya fedha na uongozi kwa kushirikiana na wakuu wa  idara na timu ya ukusanyaji mapato halmashauri ya Manispaa ya Ubungo wamefanya operesheni maalum ya kukagua leseni za biashara, leseni za vileo, kodi ya huduma ya jiji (city service levy), ushuru wa nyumba za kulala wageni ( hotel levy), ushuru wa  mabango, vibali vya ujenzi, TFDA,  ukusanyaji wa mapato na kuelimisha wafanyabiashara juu ya umuhimu wa kulipa kodi katika mitaa mbalimbali ya Kata ya Manzese.

Kamati hiyo inayoongozwa na mwenyekiti Mstahiki Meya Boniface Jacob na katibu ambaye ni Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Ndg. John Lipesi Kayombo kwa kushirikiana na watumishi hao imefanya  operesheni hiyo leo kwa lengo la kuhamasisha ulipaji wa  kodi, ada na tozo mbalimbali za Manispaa ya Ubungo.

Wakati wa  operesheni hiyo changamoto mbalimbali zimejitokeza zikiwemo wafanyabiashara kutokuwa na uelewa juu ya ukataji wa leseni, kutokukata leseni kwa wakati na kutokuweka leseni katika eneo la biashara.

Akizungumza wakati wa operesheni hiyo mwenyekiti wa kamati Mstahiki Meya Boniface Jacob aliwasisitiza wafanyabiashara kulipa kodi kwa wakati na hatimaye kuleta maendeleo katika Manispaa ya Ubungo na taifa kwa ujumla.

"Ndugu wafanyabiashara kulipa kodi ni wajibu wenu kwani itawasaidia ninyi wenyewe na vizazi vyenu na  unapolipa kodi ndipo tutaweza kujenga zahanati, shule, masoko na huduma muhimu katika Manispaa yetu" alisema Meya Boniface Jacob.

Source: michuzi blog 

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search