#Genk ya Mbwana Samatta yazidi kulisongesha !


Baada ya ukame kumuandama, Mtanzania Mbwana Samatta ameamka baada ya kuifungia KRC Genk katika uwanja wao wa nyumbani wa Luminus Arena walipofanikiwa kupata ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya AS Eupen katika muendelezo wa michezo ya plya-off ya Ligi kuu ya Ubelgiji msimu wa 2016/2017.

Magoli ya KRC Genk yalifungwa na Jere Uronen dakika ya 18 na mtanzania huyo mwenye kipaji cha kupachika vyavu kwa timu pinzani Mbwana Samatta aliyetumia vyema pasi ya nahodha wake Thomas Buffel dakika ya 58.
Kwa upande wa AS Eupen walipata goli lao la pekeekatika dakika ya 76 kupitia kwa mnigeri Henry Onyekuru, ushindi huo umeifanya KRC Genk kuendelea kuongoza Kundi B kwa kuwa na jumla ya point 19 ilizokusanya kwa kushinda michezo yake sita na kutoka sare mchezo mmoja.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search