Wajue maafisa Korea Kaskazini wanaotajwa kutengeneza makobora tishio ..soma habari kamili na matukio360..#share


Na mashirika ya kimataifa
Kim Jong-sik na Ri Pyong-chol ambao ni maafisa wa Korea Kaskazini wamewekewa vikwazo na Marekani ikidai wamechangia kuundwa kwa  makombora hatari ya nchi hiyo.
Maafisa wa Korea Kaskazini waliowekewa vikwazo na Marekani, Kim Jong-sik na Ri Pyong-chol

Wizara ya fedha nchini Marekani imesema wote walikuwa viongozi wakuu katika mpango wa makombora ya masafa marefu ya Korea Kaskazini.

Ijumaa iliyopita Baraza la ulinzi la Umoja wa Mataifa liliiwekea vikwazo vipya Korea Kaskazini  kujibu majaribio yake ya makombora ya masafa marefu.
Hata hivyo Korea Kaskazini ilisema hatua hiyo ni kama  vita.

Vikwazo hivyo vipya vya Marekani vitazuia shughuli zozote za wanaume hao wawili zinazofanywa nchini Marekani, na hata kutwaliwa kwa mali yao iliyo nchini Marekani.

Wanaume hao wawili wanaonekana mara kwa mara wakiwa na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un wakiwa maeneo ya kuyafanyia majaribio makombora.


Mwaka huu nchi hiyo imefanya majaribio kadha ya makombora tofauti ambayo inasema kuwa yanaweza kufika nchini Marekani. Tayari  nchi hiyo imetangaza kuwa na mitambo ya kuzuia makombora

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search