Kitita cha 220 Bilioni chamsubiri Coutinho Barcelona; anakuwa mchezaji ghali wa 4 katika historia ya uhamisho wa Wachezaji soka Ulimwenguni !


Mpachika mabao mahiri wa timu ya Liverpool ya nchini Uingereza Philippe Coutinho amekubaliana na offer mpya ya Timu ya Barcelona ya Spain ya uhamisho wa Pauni 76 sawa na takriban shilingi 'robo trilion' kwa pesa za 'madafu'
Kwa uhamisho huo unamfanya Coutinho kuwa mchezaji wa 4 ghali katika historia ya mpira akiwafuata kwa karibu Paul Pogba(pound 89.3), Gareth Bale(pund 85.3), na King Cristian Ronaldo(pound89). 

Coutinho anashika rekodi nzuri katika mechi zake 29 na liverpool akifunga magoli 10 na nafasi lukuki zilizozalisha magoli kwa wachezaji wenzake huku akiwa mchezaji aliepata kulipwa mshahara mkubwa zaidi katika historia ya 'the Reds'.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search