Mafuriko: Maafa makubwa ya mafuriko wilayani Lushoto..
Watu kadhaa wamenusurika kufa baada ya mawe na udongo kuporomoka na kuponda vibaya magari matatu Wilayani Lushoto, Mkoani Tanga.
Maafa hayo yametokea kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha. Watu wote waliokuwa kwenye magari hayo wamefanikiwa kutoka salama huku magari hayo yakiharibiwa vibaya.
Aidha uharibifu mkubwa wa miundombinu umejitokeza kama barabara kujaa udongo na kusababisha kukatika kwa mawasiliano katika maeneo mbali mbali wilayani humo. - Dar24
No comments:
Post a Comment