KOCHA wa timu ya Manchester United, Jose Mourinho
ambaye amegubikwa na kashfa ya usajili ya mchezaji wake nyota, Paul Pogba
inayoshuka dimbani leo kuivaa Celta Vigo katika michuano ya Ligi ya Europa,
amesema wana njia nyingi ya kucheza Ligi ya Mabingwa Ulaya - Champions League lakini ya fahari kwao ni hii ya kupitia Europa hivyo watapambana kiume uwanjani na kulitwaa kombe hilo ambalo hawajawahi kufanya hivyo.
 |
Paul Pogba |
Licha ya faida ya
bao moja la ugenini baada ya kuwalaza wenyeji wao Celta Vigo katika mechi ya
mzunguko wa kwanza iliyochezwa Hispania, Mourinho amejitapa kuwa wana nafasi ya
ushindi na pia kutinga fainali ya michuano hiyo mikubwa ya Ulaya inayofikia
kilele wiki mbili zijazo mjini Stockholm, Sweden.
"Kwa wapinzani wetu Celta Vigo hii ni mechi ya
kihistoria kwao, lakini kwetu sisi hii ni mechi muhimu,"
alisema Mourinho na kuongeza:”aijalishi tulipata nini kabla, cha muhimu
tunahitaji nini leo… Celta wana mahitaji, lakini siamini kuwa mahitaji ya Celta
ni makubwa leo kuliko mahitaji yetu."
Mourinho amesema kukosa ubingwa katika michuano mikubwa
kama hii hakumaanishi zaidi ila kunamaanisha timu yako si timu bora na isiyo na
kiwango,.. na kuikosa michuano ya Europa msimu ujao inamaanisha Man U si timu
nzuri.
“Jambo ambalo si fahari kwangu wala kwa timu yangu wala kwa
wachezaji wangu...” amewahimiza mashabiki kuiunga mkono timu ndani ya uwanja usiotabirika wa Old
Trafford.
fuatilia kikosi kamili kitakachozima ndoto za Celta Vigo kusonga mbele na michuacho hii mikubwa..
 |
Wayne Rooney |
 |
David De Gea |
 |
Juan Mata |
 |
Rashford |
 |
Michael Carrick |
 |
Ander Herrera |
 |
Phil Jones |
Ciao…
No comments:
Post a Comment