Mbowe 'apeta' kamati ya Maadili.. Halima Mdee out !!


Katika hatua ambayo haikutegemewa,. \Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge imempiga marufuku Mbunge wa Kawe jijini Dar es Salaam Mhe. Halima Mdee kuhudhuria vikao vilivyobakia vya Bunge la Bajeti linaloendelea mjini Dodoma. Hukumu hiyo imekuja kufuatia ushahidi uliojitosheleza mbele ya kamati na kujiridhisha kuwa Mhe. Mdee alidharau mamlaka ya kiti na kutoa lugha ya matusi ndani ya ukumbi wa Bunge,

Wakati huo huo, Kamati hiyo ya Bunge imemsamehe Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe baada ya kukiri kosa la kudharau Mamlaka ya Bunge April 4, 2017.
Mbunge mwingine ni Ester Bullaya ambaye amepewa karipio baada ya kukiri kosa lake sawa na Mbowe.


Hata hivyo adhabu ya Mhe. Mdee ni mapendekezo ya Kamati ambayo inasubiri baraka za Bunge kwa utekelezaji au kusamehewa.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search