'Messi feki' anusuruka kuswekwa rumande !

Kijana Reza Parastesh, raia wa Iran amenusurika kutupwa mahabusu kwa kusababisha taharuki mitaani.
Reza, ambaye ni mwanafunzi, pamoja na kuwa shabiki mkubwa wa mchezaji wa Barcelona Lionel Messi, pia anafanana naye kwa muonekano. Ikiwa ni namna ya kuonyesha mapenzi yake kwa nguli wake huyo, Reza amekuwa ananyoa nywele na hata kufuga ndevu kama Messi halisi.
Bila kujiuliza kama anayepita katika mitaa ya mjini wa Hamedan uliopo magharibi ya Iran si Messi halisi, makundi ya watu walianza kumfuata Reza kila anakokwenda ili wapige naye picha hali iliyosababisha msongamano na vurugu.
Polisi walilazimika kumwondoa Reza kutoka kwenye eneo lenye vurugu kwa usalama wake na raia waliokuwepo mahali hapo. Polisi wamempa onyo kuwa endapo hali hiyo itatokea tena basi hawatasita kumchukulia hatua za kisheria kwa kusababisha vurugu - Dar24.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search