'Vimodo' sasa baasi Ufaransa !!


Sheria nchini Ufaransa inayopiga marufuku wanamitindo wembamba wasio na afya imeanza kutekelezwa.
Wanamitindo watahitajika kuwa na cheti cha daktari kuonyesha afya yao kwa misingi ya vipimo vya uzito wao na kimo.
Wizara ya afya inasema kuwa inataka kukabiliana na matatizo ya kutokula na viwango visivyofikiwa vya urembo.
Mswada wa awali ulikuwa umependekeza uzito na kimo cha wanamitindo hatua iliyopingwa vikali na mashirika ya urembo nchini Ufaransa.
Lakini aina tofati ya mswada ulioungwa mkono na wabunge mwaka 2015 unawaruhsuas madaktari kuamua ikiwa mwamitindo ni mwembamba mno kuambatana na uzito wake umri na mwili.
Waajiri wanaovunja sheria hiyo watapigwa faini ya hadi dola 82,000 au kifungo cha miezi sita jela.

Ufaransa sio nchi ya kwanza kuweka sheria inayohusu wanamitindo wembamba- Italia, Uhispania na Israel washafanya hivyo.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search