Trump amtumbua alieanika barua pepe za Hillary Clinton..
Rais Donald Trump amemfuta kazi mkurugenzi wa shirika la ujasusi la FBI
kutokana na hatua yake ya kuliangazia swala la barua pepe za aliyekuwa mgombea
wa uraisi wa chama cha Democrat Hillary Clinton, mamlaka imesema.
Ikulu ya Whitehouse iliishangaza Washington kwa kutangaza kwamba James
Comey amepigwa kalamu.
Lakini wanachama wa Democrats wamesema kuwa alifutwa kazi kwa sababu FBI
ilikuwa ikuchunguza madai ya uhusiano kati ya Trump na Urusi.
Hatua hiyo inajiri baada ya kubainika kwamba bwana Comey alitoa habari za
uongo kuhusu barua pepe za Clinton kwa bunge la Congress wiki iliopita.
Rais Trump aliandika barua kwa bwana Comey kwamba alikubaliana na
mapendekezo ya mwanasheria mkuu Jeff Sessions kwamba ameshindwa kuliongoza
vizuri shirika hilo.
Bwana Sessions alisema kuwa idara ya haki ina nidhamu ya hali ya juu,
uadilifu na sheria na mwanzo mpya unahitajika.
Ikulu ya Whitehouse imesema kuwa utafutaji wa mrithi wake unaanza mara
moja.
Naye kiongozi wa chama cha Democratic katika Bunge la Seneti, Bwana Chuck
Schumer, amesema kuwa ni wakati mwafaka sasa kumteua kiongozi maalumu wa
mashtaka kusimamia uchunguzi huo juu ya uhusiano na Urusi.
Alisema kuwa hatua hiyo isipochukuliwa raia wa Marekani wana haki ya
kuwaza kuwa Bwana Comey amefutwa ili kupunja juhudi za kukamilisha uchunguzi
huo.
Ikulu ya White House imekanusha kuwa kutimuliwa kazini kwa Bwana Comey
kuna uhusiano wowote na maswala ya kisiasa - bbc swahili
No comments:
Post a Comment