Video: Chelsea ilipojisafishia njia UK Premier League baada ya kuibugiza Middlesbrough 3 -0




Ligi KUU ya Uingereza jana imeshika muelekeo mpya baada ya timu ya Chelsea  kutoka kifua mbele kwa ushindi wa goli 3-0 dhidi ya Middlesbrough kwenye uwanja wa Stamford Bridge.

Wafungaji wa magoli ya Chelsea ni; Diego Costa (23'), Marcos Alonso (34') na Nemanja Matic (65') .

Kwa ushindi huo, Chelsea imezidi kujihakikishia nafasi ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza msimu huu baada ya kujikita kileleni kwa tofauti ya pointi 7 zaidi mbele ya Tottenham ambapo Chelsea wamebakiza mechi 3 kabla ya kumalizika kwa msimu huu wa 2016/17sambamba na Tottenham ambao nao wamebakiza mechi 3.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search