Neno la Zari baada ya kuzagaa habari kuhusu Mahakama 'kutengua ' mazishi ya mumewe wa zamani!!



Siku ya jana Ijumaa ya tarehe 2 June, Mahakama nchini Uganda iliandika historia baada ya kutoa 'warranta' ya kutengua mazishi ya kifahari aliyofanyiwa Ivan Ssemwanga a.k.a Ze Don Ivan' ambaye pia aliwahi kuwa mume na mzazi mwenziwe na Zari ambaye kwa 'sasa ni mchumba'wa Diamond Platnumz mwanamuziki Staa wa Bongo Fleva wa Nchini Tanzania.


Katika hali iliyooenekana ni kuamsha vilio, majonzi, na simanzi kwa Zari na watoto wake watatu aliozaa na Marehemu, baada ya Mahakama kutengua mazishi ya Ivan kufuatia shauri lililofunguliwa na raia mmoja nchini humo Bw. Magugu Abey lililothibitisha pasi na shaka yoyote kwamba kitendo walichofanya Rich Gang kwenye mazishi ya Ivan cha kumzika na mamilioni ya fedha ya Uganda ni kuidhalilisha sarafu ya Nchi hiyo na kuianika Uganda machoni pa jumuia ya wafadhili ambapo dola na Randi za Afrika kusini na dola ya Marekani pia zilihusika,.. hivyo kuamuru kaburi hilo lifukuliwe na 'mtonyo' wote uachwe uingie kwenye mzunguko wa fedha ili kunyanya Uchumi.

Kabla ya Utenguzi huo wa Mahakama, Zari alilisifia sana kundi la 'The Rich Gang' kwa hatua ya kumtunza na kumuenzi Ivan na kukiita cha kumwagia fedha badala ya mashada ya maua ni cha "kiungwana na ni muhimu katika kukumbuka fadhila aliyowafanyia Waganda wakati wa Uhai wake..."


Hata hivyo, tokea jana baada ya hatua hiyo ya mahakama, Zari amekuwa kimya kama 'maji ya mtungi' wanyetishaji wakidai anatafakari 'cha kuzifanyia pesa hizo...'


Matukio bado inafuatlia kuona kama 'maelfu hayo ya mshiko' yakifukuliwa atakubali yaingie kwenye mzunguko au atasema ni mali ya watoto wake?




About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search