Wadau wa Habari waililia Mawio #share
Baraza la Habari Tanzania (MCT), Mtandao wa watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) na Umoja wa vilabu vya Habari Tanzania (UTPC) wamelaani vikali kitendo cha Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk Harrison Mwakyembe kulifungia gazeti la Mawio na kuliweka katika mzunguko kwa miaka miwili.
Tamko hilo limetolewa jana (jumapili) baada ya gazeti hilo kufungiwa juni 15 huku Waziri huyo alitumia sheria mpya ya huduma ya vyombo vya Habari ya 2016 kwa makosa ya kukiuka vifungu hivyo na agizo la Rais kutowahusisha Marais wastaafu na sakata la uporaji wa rasilimali madini.
Mratibu wa THRDC, Onesmo Ole Ngurumwa amesema hii sio mara ya kwanza katika magazeti na vyombo vya Habari kufungiwa na Waziri katika nchi yetu kwa kutumia sheria mbalimbali kandamizi hasa sheria ya magazeti ya 1976 iliyofutwa mwaka 2016 na kuridhiwa na sheria ya huduma za vyombo vya Habari.
"tunapinga utaratibu wa kisheria wa kumpa waziri mamlaka makubwa katika sekta ya habari, sheria iliyopita haina tofauti na ya sasa ya kumpa mamlaka waziri kujifungia gazeti pekee na kwa makosa atakayoyaona yeye ni kinyume na maslahi ya umma, "amesema Ole Ngurumwa.
Magazeti kadhaa yalifungiwa katika siku za nyuma ikiwemo Mwananchi, Mawio, Mwanahalisi na Mtanzania.
Tamko hilo limetolewa jana (jumapili) baada ya gazeti hilo kufungiwa juni 15 huku Waziri huyo alitumia sheria mpya ya huduma ya vyombo vya Habari ya 2016 kwa makosa ya kukiuka vifungu hivyo na agizo la Rais kutowahusisha Marais wastaafu na sakata la uporaji wa rasilimali madini.
Mratibu wa THRDC, Onesmo Ole Ngurumwa amesema hii sio mara ya kwanza katika magazeti na vyombo vya Habari kufungiwa na Waziri katika nchi yetu kwa kutumia sheria mbalimbali kandamizi hasa sheria ya magazeti ya 1976 iliyofutwa mwaka 2016 na kuridhiwa na sheria ya huduma za vyombo vya Habari.
"tunapinga utaratibu wa kisheria wa kumpa waziri mamlaka makubwa katika sekta ya habari, sheria iliyopita haina tofauti na ya sasa ya kumpa mamlaka waziri kujifungia gazeti pekee na kwa makosa atakayoyaona yeye ni kinyume na maslahi ya umma, "amesema Ole Ngurumwa.
Magazeti kadhaa yalifungiwa katika siku za nyuma ikiwemo Mwananchi, Mawio, Mwanahalisi na Mtanzania.
No comments:
Post a Comment